Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa. Kwanza nitume nafasi hii kuwapa pole familia ya Mzee Kingunge na watu wote ambao kwa njia moja au nyingine wameguswa na msiba huu na nikipe pole Chama cha Mapinduzi na niwape pole kwa dhati kabisa Watanzania ambao wanaufahamu mchango wa mzee huyu katika historia ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema jambo moja, umefika wakati kama nchi hasa Wizara yetu ya Fedha kukubali kubadili Sera zake za Kibajeti. Kwa nini nasema hivyo? Nitatoa takwimu chache ambazo ukitazama takwimu hizi zinaonekana katika taarifa za BOT za kuanzia mwaka 2011 mpaka 2017, Desemba. Hata hivyo, taarifa hizi zina complement taarifa iliyotolewa na IMF Januari, taarifa hizi sina complement taarifa iliyotolewa na Economic Intelligence Unit.

Mheshimiwa Mwenyekiti, real GDP growth yetu mwaka 2011 ilikuwa 7.9 sasa hivi tuna- project itakuwa 6.8. Hata hivyo, mzunguko wa fedha umeshuka kutoka asilimia 22 ya mwaka 2011 mpaka asilimia 1.8 ya sasa hivi. Ukiangalia Export ya hasa mazao ya kilimo ambayo ndiyo yameajiri asilimia 70 ya Watanzania, ukichukua zao la kahawa lilikuwa mwaka 2011, growth rate yake ilikuwa ni asilimia 55 sasa hivi asilimia negative 5.4.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile ukichukua cotton mwaka 2012 ilikuwa kwa asilimia 26, kwa sasa hivi imekuwa kwa asilimia hasi 3.8; ukichukua Sisal ndiyo imekuwa na ongezeko la asilimia 2.9 ya mwaka 2011, sasa hivi linakuwa kwa wastani wa asilimia 4.0; ukichukua zao la tumbaku ambalo mwaka 2011 lilikuwa kwa asilimia 56, sasa hivi mwaka 2017 kwa taarifa za BOT limekuwa kwa negative 62.7; na zao la korosho ambalo limekuwa kwa asilimia 70.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niangalie manufacturing, export ya manufacturing na hii ni business export naiongelea. Manufacturing ukichukua mwaka 2011 ili-grow kwa asilimia 96 growth rate. Sasa hivi ime-growth kwa negative asilimia 244. Tuangalie credits kwenye major economic activities; Trade, ilikuwa mwaka 2011 kwa asilimia 34 sasa hivi imekuwa kwa asilimia 16. Agro mwaka 2011 ilikuwa 51.7 sasa hivi imekuwa kwa negative 0.3. Transport ilikuwa imeshuka mpaka asilimia 22.1. Building yenyewe mwaka 2011 ilikuwa kwa asilimia 44 sasa hivi inakuwa kwa asilimia kwa wastani wa asilimia 5.0.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imports za Capital Goods zimeshuka kwa asilimia 15. Tafsiri yake ni ndogo tu. Our fiscal policies hazichochei ukuaji wa biashara na uchumi katika nchi. Nataka niwapeni mfano, takwimu zinaonesha Watanzania tunakuwa kwa wastani inasemekana asilimia mbili point something lakini ukuaji wetu wa kilimo ni 0.4 growth, hakuna matching.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hili ni jambo ambalo hata inawezekana tukasema humu ndani ya Bunge lisifurahishe upande wa Serikali kauli zetu, lakini we have a duty to tell the truth. Pia ni muhimu kabisa Wizara ya Fedha ikakubali kwamba Sera za Kibajeti za Wizara ya Fedha si rafiki katika ku-accelerate uchumi wetu kukuwa katika nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, non-performing loans, sasa hivi zimefikia asilimia 12 na hii ni taarifa ya BOT, lakini taarifa ya BOT iliyoletwa na Treasurer Registry kwenye Kamati ya PIC inaonesha kwamba mapato ya BOT yanayotokana na Trading yameshuka kwa asilimia 63. It is not a rocket science, narudia, this is just a fundamental principal kwamba our Sera za kibajeti haziwezi ku-accelerate uchumi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini ushauri wangu, jambo la kwanza ambalo namshauri Waziri wa Fedha anapoleta Mpango wake wa mwaka 2018/2019 aje na chapter inayozungumzia Tax Reforms ili tukubaliane humu ndani what is our direction. Number two, ni lazima ije chapter inayoelezea ni namna gani Agro Sector tunawekeza iweze ku-link na industrialization.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunazungumzia na tunapiga makofi jitihada zilizofanywa Serikali kwenye zao la korosho. Leo Mkoa wa Dodoma ni potential kwa ajili ya korosho. Leo Mkoa wa Tabora ni potential kwa ajili ya korosho. Swali la kujiuliza, nini mpango wa Serikali kwa ajili ya value addition kwenye mazao ya korosho. Tutajikuta tumezalisha korosho nchi mzima halafu tunategemea soko la nje la kwenda kuuza raw korosho. Tujiulize, Mwijage atengeneze clear structure ya kuonesha namna gani tunatoa incentive packages kwa viwanda vinavyobangua korosho nje vije ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna ardhi, tuna raw material na naamini tuna cheap labour, what is our problem? It’s our physical measures this is our biggest problem. Nataka nijiulize swali kwa nini tuna-charge 30 percent corporate tax kwa mtu atakayewekeza kiwanda cha mazao ya kilimo? Why? Kwa nini tunaitaka thirty percent? Kwa nini tusimwambie corporate tax zero? Kwa sababu utapata in Direct Tax kutoka kwenye Pay as You Earn, VAT na Excise Duty ambazo watu wata-spend. Why we don’t see this. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Fedha alituambia kwenye Kamati ya Bajeti na wewe ulikuwepo, alisema hivi wakati anamsindikiza Mtendaji Mkuu nadhani wa World Bank or IMF. Alimwambia nchi yenu ina bahati kubwa mbili.

Moja ya bahati tuliyo nayo ni rasilimali za kutosha tulizo nazo katika nchi. Hizi rasilimali tusiposi -turn fursa hazina maana yoyote. Kwa hiyo ushauri wangu ni lazima mentality ya Serikalini iondoke kuwaza kodi, ianze kuwaza uzalishaji.