Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nadhani nitatumia dakika chache tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema ni kwamba kama ni kwa muktadha ya taarifa ya PAC ambayo tunayo hapa mezani leo na hasa katika suala la Mradi wa Dege; taarifa ya PAC imejipambanua wazi imesema ukienda ukurasa wa 18 kwamba PAC ilishafanya kazi yake na tarehe 13 Februari, 2017 imewasilisha taarifa ya kamati ndogo ilyoundwa ndani ya PAC kwa Mheshimiwa Spika ili utekelezaji wa yale yaliyopendekezwa na kamati kuhusu Mradi wa Dege yaweze kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda ukurasa wa 44 wa Taarifa ya PAC inasema unaiagiza na kuipendekeza kwa Serikali kwamba Serikali itekeleze mapendekezo ya kamati yanayohusu Mradi wa Dege mapema iwezekanavyo ili kuokoa fedha za umma zilizowekwa katika mradi huu. Ndiyo maana nimekwambia hapa mimi nasimama wala siwezi kutumia dakika nyingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali tunaagizwa kutekeleza maagizo ya kamati tunasubiri basi Bunge tuleteeni kwasababu bado hatujapokea taarifa hiyo ili sisi tuweze kutekelezwa hayo yaliyoagizwa na Kamati ya PAC. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mara mtakapokuwa mmetuletea tutafanya wajibu wa kutekeleza lakini wakati huo tunaposubiri tumeshafanya kikao na bodi yetu ya NSSF, Bodi yetu ya NSSF tulicho waagiza ni kuhakikisha wana hakikisha ile fedha bilioni 219 ambazo ni fedha za wanachama, kama kuna mazungumzo, kama kuna jambo lolote, jambo la kwanza ni kuhakikisha bilioni 219 hazipotei ambazo ni fedha za wanachama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kuisema hapa ni kwamba PAC tunawapongeza, mnaendelea kufanya kazi zenu kwa utaratibu unaotakiwa. Kwa hiyo, mara mtakapotukamilishia, mkatuletea ripoti na mkaona ripoti hiyo inatakiwa ije Serikalini ili Serikali tutekeleze yale mliyoagiza sisi kama Serikali tuko tayari na tunawasubiri; tuleteeni tuweze kuchukua hatua mtakazozisema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niendelee kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge, jana tumetunga sheria ya kuunganisha mifuko na nilishawaambia kwamba kwenye suala la madeni ya Serikali kwenye mifuko na hasa fedha ambazo zinahusu michango ya wanachama Serikali tayari imeshalipa trilioni 1.3 ili kuhakikisha kwamba michango ya wanachama inakuwa salama. Masuala mengine tunamwachia Mheshimiwa Waziri wetu wa fedha ataendelea kuyafanyia kazi kwa utaratibu unaotakiwa

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naomba niokoe dakika zako, kwa sababu haya ndiyo yaliyojiri kwenye sekta ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ninakushukuru kwa kunipa muda.