Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza awali ya yote napenda sana kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha mwaka huu wa 2018 na hili ni Bunge letu Tukufu tumekutana Bunge la Wabunge wenyewe kwa sababu ndiyo Kamati za Bunge zinawasilishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kupongeza Kamati zote mbili na nipende kuwapongeza kwa dhati ya moyo wangi Wenyeviti wa Kamati na Wajumbe wao wote. Mimi nashukuru sana Kamati ya LAAC tumekaa muda mrefu sana tukijadiliana, kwa kweli imetupa mwongozo mkubwa sana wa nini tunatakiwa tufanye katika kuhakikisha kwamba tunazisimamia vizuri Halmashauri zetu. (Makofi)

Mgheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika kamati ya LAAC nimekuta hoja hii ya fedha za ALAT ambazo zimetumika kinyume na taratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli chombo kile huko nyuma kilikuwa hakiendi vizuri na ndiyo maana hivi sasa kuna timu imeundwa na leo hii Kamati Tendaji ya ALAT Taifa iko hapa Dodoma kwa ajili ya kupitia repoti ya ukaguzi maalum iliyofanywa. Lengo lake ni kwamba yale yatakayobainika hatua mbalimbali ziweze kuchukuliwa. Kwa hiyo, ni jukumu la Serikali kwamba inapopata repoti kuhakikisha inafanyakazi vya kutosha kuhakikisha kuondoa machafu yote. Sisi tumejipambanua, ajenda yetu ni kuhakikisha kwamba pale kwenye maovu ya aina yoyote tuweze kuyafanyia kazi kwa mustakabali mpana wa rasilimali za nchi yetu ziweze kukaa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli taarifa ya Mkaguzi Mkuu imeeleza suala zima la manunuzi yasiyozingatia Sheria na utaratibu na kweli hili lilitokea huku nyuma. Kamati ilizibainisha wazi, na halmashauri mbalimbali zilizoitwa pale kuna maelekezo mengi yalitolewa. Hata hivyo jukumu letu sisi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa katika hilo, tuliweza kuchukua hatua mbalimbali kwa wale wote ambao walikiuka taratibu. Tumechukua hatua takribani kwa watumishi wapatao 434, kati ya hao tisa wamefukuzwa kazi, 210 wamepewa maonyo mbalimbali, watumishi 15 wapo katika vyombo vya dola, lakini 28 wamesimamishwa kazi kwa ajili ya uchunguzi, wapatao 64 wako katika hatua ya uchunguzi mbalimbali za kiupelelezi, 13 wametakiwa kulipa fidia hasara waliyoisababisha katika maeneo yao hali kadhalika watumishi wanne wameshushwa vyeo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo kubwa la hili ni kutekeleza yale ambayo yamebainishwa katika repoti mbalimbali. Hili ni jukumu letu, lazoma tuweke nidhamu katika nchi yetu. Kwa sababu Halmashauri zetu; kwa mfano tukichukua bajeti ya mwaka huu ya trilioni 31.7 karibu trilioni 6.58, asilimia 20.7 ya total budget iko katika halmashauri zetu. Kwa hiyo tusiposimamia vyema tutaliangusha taifa hili. Kwahiyo naomba niwashukuru Wajumbe wa Kamati, na maagizo mbalimbali tunaendelea kuyafanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajenda nyingine ni kuhusu ukusanyaji wa mapayo. Ni kweli Halmashauri zetu huko nyuma tulikuwa tunakusanya watu wanasema kwa zile receipt za ngalawa. Sasa kuna maelekezo mbalimbali ya jinsi ya kutumia mifumo ya electronic katika Halmashauri zetu. Katika jambo hili tumefanya hatua mbalimbali na hasa kuzihimiza Halmashauri zijirekebishe katika ukusanyaji wa mapto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru tunapozungumza Halmashauri zote 184 zimeshaingia katika mifumo huo wa ukusanyaji wa mapato. Kwa hiyo hii ofisi yetu imehakikisha kwamba inetekeleza agizo hili, vilevile Kamati wanafaham. Katika hatua mbalimbali Kamati ya TAMISEMI na Kamati ya LAAC tumeendelea ku-report kwamba tumeweza kutekeleza katika yale ambayo maeneo hapo awali yalikuwa na mapungufu makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo naomba niwaombe Wabunge wenzangu, sisi tukiwa kama Madiwani katika Halmashauri zetu, hata hii mifumo ikiwepo bado kuna watu wengine wana-divert kutoka katika mifumo hii. Badala ya watu kuhakikisha tunasimamia lakini kuna watu wengine wanatumia mifumo mingine kwa sababu wameshazoea ubadhirifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe sana mifumo hii sasa ipo, tusisitize katika Halmashauri zetu na kuhakikisha wale ma-accounting officers katika Halmashauri zetu na wasimamizi wao wote wa chini wahakikishe fedha zinakusanywa, zinaingia katika mfuko ili hatimaye tuweze kupata mafanikio makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na nyinyi mnafahamu, hata katika sekta ya afya kwa kutumia mifumo leo hii tumepata faida kubwa sana. Hospitali zilikuwa zinakusanya wastani wa shilingi 150,000 mpaka 200,000 kwa siku lakini leo hii wanakusanya kuanzia milioni moja mpaka milioni 1.5 kwa siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna variationkubwa sana, ukiangalia hospitali nyingine kwa mwezi wanakusanya takriban wastani wa shilingi milioni nne sasa wanakusanya milioni ishirini na sita mpaka milioni arobaini. Kwa hiyo mfumo wa ukusanyaji wa mapato; na mimi niwashukuru sana Kamati zote, Kamati ya LAAC kwa ajili ya kubainisha hili na kutoa maelekezo na Kamati ya TAMISEMI inayotusimamia katika jambo hili. Tumepata mafankio makubwa; na mimi nina imani tutaendelea kuweka msingi mzuri wa ukusanyaji wa mapato katika maeneo mbalimbali

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajenda nyingine iliyobainishwa ni suala la mikataba. Kwamba kuna usimamizi mbovu wa mikataba; na ndiyo maana naomba niwaambie kwamba sisi ofisi yetu baada ya kuona hili sasa tumejikita katika kusimamia mikataba. Naomba niwaambie kwamba tumeshaanza kuchukua hatua mbalimbali na ninyi wenyewe nio mashahidi. Hata mwaka huu kama mlivyoona kwamba suala la mikataba inayokiuka utaratibu, hasa kule Nkasi tumemsimamisha Mkurugenzi kwa ajenda tu hii ya usimamaizi wa mikataba; pamoja na maeneo mbalimbali. Mmesikia maeneo hata Butiama juzi tumemsimamisha Mkurugenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo sasa hivi tunawafanyia vetting Wakurugenzi ambao wanashindwa commitment zao za kazi. Ndiyo maana hata ndugu yangu pale Nape ameshika shavu hapa ananisikiliza, niwaambie tu kwamba nafanya kazi kweli kweli tunahakikisha kwamba tutafanya vetting, na Mheshimiwa Rais ameteuwa hawa Wakurugenzi wana uwezo mkubwa. Hata hivyo lakini wale watakaobainika baada ya kuona kwamba mambo mengine hayaendi vizuri si jukumu la Serikali hii kuvumilia watu ambao wanashindwa kutimiza wajibu wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la miradi ya maji. Ni kweli, na bahati nzuri kaka yangu Engineer Kamwelwe amelizungumza hapa; tutalisimamia. Waheshimiwa Wabunge mnafahamu huko tulikopita kuna maeneo mengine wakandarasi wengine tumewatoa katika miradi hii ya kazi. Lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba tunapata wakandarasi ambao wako competent. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na tatizo lingine la wasimamizi, wakandarasi na washauri. Wakati mwingine kulikuwa na negosiation inafanyika kuhusiana na miradi hii ndiyo maana ilikuwa inaenda vibaya. Mnakumbuka tulivyokuwa Korogwe kule nilimuomba Mheshimiwa Rais atupatie fursa ya ku-blacklist wakandarasi wote wa miradi ya maji, hali kadhalika miradi ya barabara ambao wanakwamisha. Naomba niwaambie hili zoezi sasa hivi linaendelea na si muda mrefu mtaona watu mbalimbali wakili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba niwasihi Wabunge. Kuna wakandarasi wengine ni marafiki zetu. Wakati tunawashughulikia naomba mtuache tuwashughulikie kwa nidhamu ya nchi hii, kwa sababu hatuwezi kukubali fedha ambazo zinaenda kwa wananchi kuna watu wengine wanazifanyia mambo ya hovyo ambayo hayakubaliki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili suala zima la asilimia tano. Ni kweli kwamba historia ya huko tulikotoka hii asilimia tano ilikuwa haiendi vizuri. Wale walio katika Kamati ya TAMISEMI wanafahamu kwamba tuliitengeneza bajeti guideline, kwamba lazima kila Halmashauri itenge asilimia tano kwa vijana na asilimia tano kwa akina mama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha uliopita takribani shilingi bilioni 19 kwa mara ya kwanza ziweze kufika katika Halmashauri zetu. Mwaka huu tuna zaidi ya shilingi bilioni sitini na moja kwa bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017, 2017/2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Zitto amezungumza hoja hapa, leo hii tuna Bodi yetu ya Serikali za Mitaa; nimewaambia wataalamu wetu, kwamba fedha hizi kwa Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa tunaweza tukatengenezea utaratibu na tukaweka mfumo mzuri ili Halmashauri zetu zipeleke huko moja kwa moja kwa utaratibu mzuri ili watu waweze kukopa na hatimaye compliance ya ulipaji wa madeni iweze kuwa vizuri. Watu wanaona hizi fedha zinatolewa kama sadaka, hapana hizi fedha zimelengwa ni kwaajili ya kuwasaidia wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nishukuru sana, katika mwaka huu wa fedha Waheshimiwa Wabunge mbalimbali wamesimama hapa kushuhudia yaliyotokea leo hii katika Halmashauri nyingi. Hii ni tofauti na yaliyotokea nyuma ambayo ripoti hii leo tunaijadili. Kwa kiwango kikubwa maeneo mengi watu wameendelea kufanya vizuri. Katika hili niwasihi Waheshimiwa Wabunge fedha hizi siku zote nasema zinabaki katika Halmashauri zetu kule kule hazifiki kwa Dkt. Mpango, hizi ni Kamati ya Fedha kila mwezi tunakusanya mapato yetu. Naomba tusaidiane katika kuhakikisha kwamba tunasimamia fedha hizi ili vijana wetu na akina mama katika maeneo hayo waweze kupata fursa ya mikopo ambayo itawasaidia katika uwekezeji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndiyo maana ile ajenda yangu ya kusema viwanda vidogo 100 katika kila mkoa; tena nilisema viwanda vidogo vidogo na maana yangu ni kwamba kiwanda kidogo unit price ya kiwanda kidogo kina range kati ya shillingi milioni tano mpaka milioni kumi. Ukija katika bajeti yetu ya takriban shilingi bilioni sitini plus. Ukizungumza unit price ya kiwanda cha wastani cha milioni 10 unazungumza viwanda takribani 6000 hata nusu ya pesa hiyo ikitoka karibuni bilioni 30 unazungumza karibuni viwanda 3000 tume- outstand expectation ya viwanda 2600 kwa mikoa yote. Kwa hiyo, nilizungumza target ile ili viongozi tuweke leadership ya kuhakikisha tunawahamasisha watu wetu, ambao wengine ni wadogo wadogo wanataka kusaidiwa. Hii ni sehemu ya employment kwake la kumuwezesha kufuka katika suala zima la kimaendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuhakikisha maagizo ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali zinafuatiliwa, jambo hili tumelichukulia hatua kali sana. Tumewaagiza Wakurugenzi wote kwamba tutawapima kwa utekelezaji wa maagizo ya CAG. Jambo hili nimeripoti mpaka katika Kamati na tuko firm katika hili; na naomba niwaambie mtaona kundi kubwa la Wakurugenzi tutawaondoa katika nafasi zao, wale wataoshindwa ku-meet target ambayo tumewaelekeza; kwa sababu nikijua hapa hii ndiyo sehemu ambayo inaenda kujibu matatizo ya wananchi wetu ili hatimaye waone kwamba maeneo mbalimbali wananchi wanapata fursa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa fursa hii, ahsante sana.