Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami naomba nianze kwa kweli kwa kuwapongeza Wenyeviti na Wajumbe wa Kamati hizi sababu wamegusa maeneo muhimu sana kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu na hususani wote kwa pamoja ni lazima tupambane na ubadhirifu dhidi ya matumizi mabaya ya fedha za umma katika Serikali Kuu pia katika Serikali za Mitaa. Wamefanya kazi nzuri sana wanastahili pongezi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maeneo ambayo ningependa nitoe ufafanuzi kidogo

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na suala la Benki ya Azania, ni kweli Benki ya Azania pale tuna tatizo na tatizo lenyewe ni la kisheria. Benki hii ilisajiliwa kwa Sheria ya Makampuni Sura 212. Kwa hiyo, kwa usajili huo inakuwa ni kampuni binafsi na CAG hawezi kui-audit hata kama inamilikiwa kwa takribani asilimia 92 ya hisa zinashikiwa na mifuko yetu. Kwa hiyo, huo ndiyo utata ulipo ingawa benki hii imekuwa inakaguliwa pia na makampuni ambayo CAG kwa nyakati tofauti anayatumia pia kukagua taasisi mbalimbali kwa niaba yake na wanawasilisha taarifa kwake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wamewahi kukaguliwa KPMG, PWC na hivi sasa wanakaguliwa na Ernst and Young. Kwa hiyo, jambo kubwa hapa ninachofikiri ni kwamba CAG wakati utata huu wa kisheria unafanyiwa kazi ni vema angeanza kuzitazama hizi audit report ambazo zinakaguliwa na Ernst and Young.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Pride sijui naweza nikalisema kiasi gani, kwa kifupi ni kwamba hili shauri limepelekwa Mahakamani, liko Mahakama ya biashara na limepangiwa kusikilizwa mwezi Machi tarehe za mwanzoni. Mengine yanayosemwa pengine ni magumu hayapendezi sana labda niyaache kwa sababu ni shauri ambalo liko Mahakamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa kulisemea ni kuhusu fedha za maendeleo kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa. Fedha hizi tumejitahidi kutoa kulingana na makusanyo ambayo yamepatikana katika kipindi cha miezi sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa fedha za ndani mpaka kufikia mwezi Desemba tulikuwa tumetoa shilingi bilioni 165.96 ikilinganishwa na lengo la miezi sita la kutoa bilioni 264.8. Maana yake kwa nchi nzima tayari tumekwisha kutoa takribani asilimia 63 ya lengo la nusu mwaka.

Kwa upande wa fedha za nje tulitoa bilioni 205.93 ukilinganisha na lengo la bilioni 174.5, hiyo ni asilimia 118 ya lengo. Nadhani ni vizuri hizi takwimu zikafahamika Mzee wangu Mheshimiwa Lubeleje nikitoa mfano wa Mpwapwa fedha za ndani, Mpwapwa DC walipatiwa shilingi milioni 884.1 wakati lengo ilikuwa ni bilioni 1.48 hii ni asilimia 60. Fedha za nje walipatiwa milioni 606.2 wakati lengo lilikuwa ni milioni 469 hii ni asilimia 129, naweza nikaendelea kutoa mifano mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano OC ya Babati tumetoa milioni 394 kati ya lengo la milioni 465.9 hii ni asilimia 85 kwa Babati TC. Kwa upande wa DC tumetoa mlioni 808 wakati lengo lilikuwa ni milioni 901.9, na hii ni asilimia 90 kwa ajili ya Babati DC kwa OC. Kwa hiyo siyo kweli kwamba hatujatoa fedha, tumetoa fedha. Fedha zinakwenda lakini kwa quarter ya kwanza nakiri kuna tatizo la upatikanaji wa fedha na hapo ndiyo kuna slow down lakini sasa zimeanza kufika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na hoja imesema kwamba CAG hapewi fedha; nadhani ni vizuri tuwe tunajiridhisha na takwimu. Kwa upande wa OC Vote 45 kwa miezi sita tumempatia bilioni 17.8 kati ya lengo la bilioni 22.2, kwa hiyo kwa miezi sita amepatiwa asilimia 80 ya lengo. Upande wa development ni kweli tumechelewa lakini fedha za nje tayari amepatiwa asilimia 41 ya lengo la development katika kipindi hicho. Kwa hiyo ni vizuri nadhani tuwe tunaziangalia hizi namba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Heche alini- challenge na mimi ngoja nim-challenge kidogo. Kwa miezi sita upande wa property tax tumekusanya shilingi bilioni 16.6. Sasa makusanyo ya TRA peke yake kwa mwezi mmoja ni wastani wa trilioni 1.2 kwa hiyo hesabu iko wazi kabisa siyo kwamba hiki chanzo ndicho the major source ya mapato ya Serikali hata kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kodi ya majengo, sisi tunaongozwa na kifungu cha 65(b) cha Sheria ya Fedha ambayo Bunge hili lilitunga mwaka jana na kinaelekeza kwamba fedha hizi zikusanywe na TRA moja na kuhifadhiwa kwenye Mfuko Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ni kwamba mgawanyo wa utoaji wa fedha uendane na bajeti ya Halmashauri husika. Na takwimu nilizoanza kuzitoa kwa maana ya fedha ambazo tumepeleka kwenye Halmashauri zinafuata utaratibu huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme pia kuhusu utendaji wa Benki ya Kilimo Tanzania. Ni kweli hili lina matatizo na Serikali imeliona na imeanza kulifanyia kazi. Tayari tumekwisha kutafuta management mpya kwa utaratibu wa search na tayari wamefanyiwa interview na kwa hiyo, baada ya muda mfupi kwanza tunabadilisha management. Na kwa upande wa mtaji ni kweli mwaka 2014 ndipo Serikali ilitoa shilingi bilioni 60 kama mtaji, lakini baada ya hapo tulitoa shilingi bilioni 206 ambazo ulikuwa ni mkopo nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika. Kwa hiyo, suala la mtaji kwa ajili ya Benki yetu hiyo ambayo ni muhimu…

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani hayo mengine asubiri kesho, Serikali inatoa fedha kuendana na bajeti. Kama Bunge hili lilipitisha kiasi fulani kwa ajili ya Ofisi ya CAG ndizo hizo tunafanyakazi tukishakusanya tutampa hizo na siyo zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naeleza juu ya TADB (Benki ya Kilimo) kwa hiyo mbali ya zile bilioni 60 ambazo tulitoa mwaka 2014, tulitoa pia bilioni mia mbili na sita ambazo tulipata mkopo nafuu kutoka African Development Bank. Baada ya kuimarisha utendaji katika Benki hii hapo ndiyo tutaendela kushughulikia suala hili la mtaji maana hatutaki pia tuendelee kupeleka mtaji ukazame kama kwenye shimo na kupoteza fedha za umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nitapenda kulisema ni fedha ambazo TRA inakusanya kwa ajili ya taasisi mbalimbali. Tunakusanya fedha kwa mfano, wharfage kwa ajili ya TPA lakini pia ziko fedha kwa ajili ya REA, Road Fund, maji; hizi kwa ujumla hazina matatizo. Hazina matatizo kwa sababu marejesho yake yako kwenye bajeti ya matumizi (Appropriation Bill), na hizi zinatolewa kuendana na utaratibu wetu wa mgao wa kila mwezi. Shida inapoonekana sanasana ni kwenye maeneo mawili; kuna bed night levy kwenye utalii na cashewnut levy kwa upande wa korosho asilimia 35. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa fedha zote hizi zinaingizwa kwenye mfuko mkuu wa hazina. Sisi tunachosisitiza ni kwamba ni muhimu sana tujiridhishe na matumizi ya fedha hizi. Fedha hizi mnajua, mifano ni mingi boards zilizokuwa zinakaa nje ya nchi mnafahamu, Kamati ya PAC imetoa mfano wa fedha za ALAT ambazo zimekuwa misused.

Kwa hiyo, ni muhimu sana kwamba fedha hizi zionekane kwenye bajeti ya matumizi na kwahiyo ziombewe na kugawiwa kama utaratibu mwingine unavyofanya. Kwa hiyo hili nadhani shida iko hapa lakini tumelimaliza kwa uoande wa korosho tayari Serikali imeshawapatia shilingi bilioni 10 na kwahioyo pale watakapoleta matumizi mengine yakachambuliwa watapewa fedha wka utaratibu wa kawaida maana wameshaingizwa kwenye mfumo rasmi wa matumizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi.