Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia angalau kwa mambo machache ambayo nimeyapitia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa fursa hii ya kusimama mbele ya Bunge leo kuchangia nikiwa kama mmoja wa Wajumbe wa Kamati zilizowasilisha ripoti zake leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na namna ambavyo CAG ametuonesha matumizi mabaya ya Ofisi ya ALAT. Ni ukweli usiopingika kwamba chombo cha ALAT kinachounganishwa na Halmashauri zote nchini, kinapokusanya fedha zake kinakusanya fedha kwa lengo la kuendesha chombo hiki na kila Halmashauri nchini inachanga fedha kwa ajili ya chombo hiki kuendeshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka michache iliyopita ALAT ilikusudia kujenga jengo kwenye Mji wa Dodoma lakini kama CAG alivyotuonesha, kwenye milioni 523 kati ya fedha hizo milioni 367 hazionekani wapi zimekwenda. Kamati ya PAC imeliona hili na kulileta kwenye Bunge lako ili Bunge lako liweze kushauri vinginevyo lakini kuchukua hatua stahiki juu ya fedha za wananchi kutoka kwenye Halmashauri zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niende haraka haraka kidogo kwa sababu najua muda wangu ni mchache. Lipo suala la urejeshaji wa fedha kutoka TRA kwenda kwenye taasisi mbalimbali za Serikali, tulitamani sana kama ambavyo makubaliano na mujibu unavyotaka fedha zote zinazokusanywa kutoka Halmashauri, kutoka wapi, inapofika wakati kwa mujibu wa sheria na misingi ile ya kuendana na bajeti zilizopangwa, fedha hizi ziende kule kwenye halmashauri zikafanye kazi yake sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa kidogo, hawa Wakurugenzi wanaopigwa mawe hii tabia ya kuzungumza unaenda mbele unarudi nyuma, ndugu yangu, Mheshimiwa Heche amesahau kidogo, dakika chache zilizopita Mheshimiwa Gekul hapa ametupa mfano bora watu tukajifunze Babati kwamba pale kuna Mkurugenzi makini anayefanya kazi yake sawasawa. Sasa matatizo ya mtu mmoja hayawezi kujumlisha Wakurugenzi zaidi ya 168, ni lazima tukubali na twende na kauli hiyo, itatusaidia kujenga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa PAC Mheshimiwa Heche amezungumza hapa habari za NIDA, habari za vitambulisho na kadhalika. Kamati ya PAC ilipokuwa inapitia taarifa zake mbalimbali, zipo taarifa zitakuja kwa wakati mahsusi na yapo mambo kama hayajakamilika hayana sababu ya kuja kwenye Bunge hili! Hii ni sambamba na taarifa ya mradi wa Dege, Kamati imeunda Kamati ndogo imetengeneza taarifa zake vizuri imepeleka kwa Spika zimeanza kufanyiwa kazi, Bunge tusubiri taarifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ni lazima tukubali. Umezungumzwa hapa mradi wa Mlimani City, umetajwa mradi wenye maajabu saba, ni kweli. Mradi wa Mlimani City leo una takribani miaka 11, mradi huu toka uanzishwe tunataka kusema pamoja na changamoto zake ambazo CAG ameziona, kama Kamati tumezielewa. Siyo hili tu la mradi mbovu, tunaongelea habari ya Chuo Kikuu cha Mlimani kinachotoa wataalam waliobobea, kinachotoa ma- Profesa, leo ametajwa humu Waziri wa Sheria, Mheshimiwa Profesa Kabudi pale na wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi leo mimi niwaulize kwa makosa ya mtu mmoja kuingia mikataba mibovu, mnataka kusema watu wote waliopita Chuo Kikuu cha Mlimani uwezo wao ni dhaifu? Kwa sababu ni lazima tukubali changamoto hizi zipo na kama changamoto hizi zipo, kwa mfano, mradi huu toka ulipoanzishwa sote tunafahamu zipo faida kubwa zimeonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulipojengwa mradi wa Mlimani City tunaamini eneo lile limeongezeka thamani, pamoja na matatizo ya Mlimani City sote tunafahamu miaka 11 iliyopita ukirudisha miaka minne nyuma, Chuo Kikuu cha Mlimani kimekuwa kikipata bilioni 16 na pointi kama gawio kutoka Chuo Kikuu, fedha hizi zinaiwezesha Mlimani City kujihudumia kwenye bajeti yake kwa asilimia 28. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukifanya hesabu ya kawaida sote tunakubali Mlimani City ina matatizo ya kimkataba na waliohusika wapo na hatua zimeshaanza kuchukuliwa baada ya CAG kutoa ripoti hii. Tunachokisema sasa Serikali baada ya mradi huu tutulie twende polepole, tunaongea facts hapa, hatupigi kelele, tunaongea facts hapa! Serikali kila mwaka inapata kodi ya VAT… (Makofi)

(Hapa baadhi ya Wabunge waliongea bila mpangilio)

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Serikali kila mwaka inapata kodi ya VAT bilioni 18 kutoka Mlimani City kwenye biashara zote zilizopo pale. Sote tunakubali property tax takribani milioni 150, lakini tax levy ya Manispaa ya Ubungo zaidi ya milioni 72. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachosema, Kamati imebaini matatizo kwenye Mkataba wa Mlimani City. Tunaiomba Serikali iangalie na ifanye kazi vizuri kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naomba Bunge lako liweze kuunga mkono.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.