Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wakati Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli anaingia madarakani miongoni mwa miradi ambayo aliwatangazia Watanzania na dunia kwamba ni miradi ya kifisadi ni mradi wa NIDA, mradi wa vitambulisho vya Taifa wa NIDA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unakumbuka wakati akina Dickson Mwaimu wanawajibishwa, Rais Dkt. Magufuli alisema kwamba kitambulisho cha kupigia kura ambacho kilikuwa na ubora kuliko kitambulisho cha NIDA kilitengenezwa kwa Sh.3,000 na akasema kwamba vitambulisho milioni 23.5 vya kupigia kura vilitengenezwa kwa bilioni 70.

Mheshimiwa Mwenyekiti, akawa anashangaa inawezekana vipi kitambulisho cha kupigia kura ambacho kina ubora kuliko wa NIDA kikatengenezwa kwa bei ya chini huku kitambulisho cha NIDA kikitengenezwa kwa Sh.17,000 na akina Dickson Mwaimu wakachukuliwa hatua sitaki kwenda huko. Akampeleka pale mtu anaitwa Ndugu Kipilimba, kukaimu nafasi ya Ndugu Dickson Mwaimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitambulisho kile ambacho kilikuwa Sh.17,000 kikapanda kwa kampuni ile ya kwanza iliyotuhumiwa kupewa tenda kuongezewa muda, kampuni iliyotuhumiwa kutengeneza kitambulisho kwa bei ya juu na watu wakachukuliwa hatua, ikatengenezwa addendum ikaongezewa muda kisanii na kitambulisho hiki kikapanda kutoka Sh.17,000 mpaka Sh.26,000. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nahitaji maelezo ya Serikali na Mwenyekiti wa Kamati atuambie ilikuwaje taarifa hii ikaondolewa? Huu ni ufisadi na siku zote tumesema kwamba Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi inalea ufisadi na inajaribu kufunga watu midomo wasiseme ufisadi unaotokea wakati huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili jana…

T A A R I F A . . .

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naongea mambo mazito sana sitaki kufanya comedy hapa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo nahitaji maelezo, siku zote na Watanzania wajue kabisa kwamba kuna mambo mengi tu yanafanyika kwenye Serikali hii ambayo yana ufisadi kuliko hata Serikali zilizopita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kitu ambacho kimezinduliwa jana kinaitwa E-Passport, huko nyuma uliwahi kufanyika utafiti wa jinsi ya kuleta kitu kinaitwa E-Migration, E-Migration ilikuwana zaidi ya components sita, ilikuwa na E-Passport, E-Visa, E-Border na E-Visa kitu kikubwa kilichokuwa mle ni kwamba mtu anapokata visa akiwa hata Marekani vituo vyetu vya immigration hapa nchini watu waweze kusoma na wakajua ili kudhibiti mapato. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana imezinduliwa E- Passport na ule mradi mzima uliokuwa na components sita ulikuwa ni wa dola milioni 180, jana imezinduliwa kitu kinaitwa E-Passport ambacho kina component moja tu kwa dola milioni 50, tenda yake hatujui imetangazwa lini, nani na nani walioshindanishwa. Hii nchi ina sheria na taratibu, tunaruhusu vipi nchi yetu hii miradi ya kifisadi inatokea kila leo, kila kesho na Serikali hii inayojinasibu kwamba inashughulikia ufisadi watu wachache wanatengwa wengine wanaruhusiwa kuendelea kupiga ufisadi kwenye nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Serikali za Mitaa.

Amezungumza hapa Mheshimiwa Bobali kwamba Serikali za Mitaa Wakurugenzi waliowekwa ni Wakurugenzi ambao ni dhaifu na wengi ni walioshindwa uchaguzi katika kura za maoni za CCM. Mimi sitaki kulizungumzia hili, nataka tu nimwambie rafiki yangu, Mheshimiwa Bobali, haya ni makusudi ya Serikali hii kuua Serikali za Mitaa, imekusudia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana hata wakati watu wanazungumza hapa kuhusu Wakurugenzi na matatizo ya Wakurugenzi, amezungumza hapa Mheshimiwa Mzee Selasini, hakukuwa na Waziri hata mmoja hapa anayeshughulika na hilo, kwa sababu nia yao ni kuua hizi Serikali za Mitaa. Ndiyo maana hata mapato ya Serikali za Mitaa yametolewa na hayarudishwi. Mapato ya mabango, kodi za nyumba zilizokuwa zinakusanywa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nam-challenge kaka yangu pale atuambie, mkitoa pesa mnazochukua kwenye mabango ninyi mapato yenu ni kiasi gani, mtuambie ni shilingi ngapi mnazopata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.