Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na kauli mbiu ya Serikali ya viwanda ni vyema tukaboresha Benki ya Kilimo na kuifikisha mikoani ili wakulima waweze kukopesheka ili waweze kujikomboa kimaisha na kufikia malengo ya viwanda katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu soko la uhakika la mazao, kutokana na nchi yetu kuwa na idadi kubwa ya wananchi ambao ni wakulima wamejikita kwenye kilimo cha mazao ya chakula na mazao ya biashara ambayo yamekosa soko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sekta binafsi, Serikali inapaswa kushirikisha sekta hii katika taratibu za kukuza uchumi katika nchi yetu ili waweze kuwa mfano na wengine waweze kuwekeza katika nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sekta ya maliasili na utalii, kulingana na umuhimu wa sekta hii ya utalii ni muhimu ikatazamwa kwa umakini mkubwa kwani tukiwekeza kwa kufanya tafiti za kutosha tutaweza kupata fedha nyingi za kigeni kwa kutengeneza mazingira rafiki kwa watalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya kilimo ipewe kipaumbele katika shughuli zote za maendeleo kwa kuwawezesha wakulima kwa kuwapa pembejeo, mtaji na elimu ya kuachana na kilimo cha mazoea badala yake kiwe cha kisasa. Kuhusu kilimo cha umwagiliaji, Serikali ijielekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji ili kuelekea kwenye nchi ya viwanda kuepuka kilimo cha msimu ambacho hakitabiriki na kinaweza kisifikie malengo ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa sekta ya madini, kulingana na umuhimu wa viwanda ni vyema Serikali ikawekeza kwenye utafiti ili wanavyuo wanapomaliza masomo yao waweze kusaidia Taifa la Tanzania kwa upande wa madini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Deni la Taifa, ni vyema kama Taifa tukawa na utaratibu wa kukopa mikopo ambayo haiwezi kuwatesa Watanzania wote. Tutaweza kuepuka kero hiyo kwa kukopa kwa wazabuni wa ndani ambayo haitakuwa na kero kubwa.