Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mungu kunipa nafasi ya kuchangia hoja iliyopo mezani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanafunzi wanaopata nafasi ya kujiunga na masomo ya elimu ya juu wamekumbana na changamoto ya kupata mikopo, hasa wanafunzi wenye mahitaji. Ninatambua pia umuhimu wa kutoa fursa zaidi kwa wanafunzi wanaochukua masomo kusomea taaluma zenye upungufu, sayansi etc.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapendekeza Sera ya Elimu ya Juu na Kanuni zake zipitiwe upya, kwa sababu wanafunzi wanaofaulu kwa kiwango cha juu kidato cha sita ni wale waliosoma shule binafsi zenye mazingira mazuri ya kujifunzia, walimu, vitabu, maabara na kadhalika, matokeo yake, hao wenye uwezo ndio wanapata mikopo wakati si wahitaji. Karo za shule walizosoma ni ghali kuliko ya vyuo vikuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, lile lengo la kutoa mikopo kwa wahitaji na wanaotoka kwenye familia zenye uchumi mdogo/duni, halikufikiwa. Kwa wakati huu, utaratibu wa kutoa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu ufanyiwe mapitio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.