Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JANETH M. MASSABURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira mwingi wa rehema ambaye yeye ndiye amenipa kibali kuwa katika Bunge hili leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kipekee naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wetu mpendwa wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania kwa kuniamini na kuniteua kuwa Mbunge katika Bunge lako Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Spika pamoja na ninyi Wenyeviti wote. Kwa kipekee vilevile niwashukuru Wabunge wote kwa mapokezi mazuri na upendo waliouonesha kwangu. Naomba Mwenyezi Mungu azidi kuwabariki Wabunge wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tuzidi kuwatetea wananchi wengi wa Tanzania walio wanyonge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikishukuru chama changu, Chama cha Mapinduzi, chama chenye kuleta matumaini kwa Watanzania hasa wanyonge kwa kunilea vyema na kunishauri, na hapa nilipo ni Chama changu cha Mapinduzi ndiye mlezi thabiti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuishukuru familia yangu, wazazi wangu, watoto wangu, shemeji zangu, majirani ndugu na marafiki kwa kunilea na kunipa moyo na hasa wakati mgumu nilipoondokewa na rafiki yangu mpenzi wangu Didas Massaburi. Mwenyezi Mungu azidi kumpokea katika makao yake ya milele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango huu mimi nimeona kuna mambo mazuri mengi, lakini si maana kwamba yote ni mazuri tu na ndiyo maana kuna miaka mitano ya kujisahisha na ndiyo maana kuna bajeti za kila mwaka, penye mapungufu unajaza, unatoa wazo la kuleta manufaa.

Katika mpango wa miaka mitano (2016/2017 - 2020/ 2021) wametenga kanda tano maalum za kiuchumi. Kuna eneo maalum la uwekezaji la Bagamoyo hilo liko Mkoa wa Pwani, lengo kuu ni kujenga bandari ya kisasa ambayo itaruhusu meli kubwa na eneo hili litakuwa lango kuu la biashara za kikanda na kimataifa, lakini kutakuwa pia na viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kituo cha viwanda cha Kurasini Dar es Salaam. Mradi huu pia utaimarisha ushirikiano wa kibiashara kati ya Tanzania na mataifa mengine kupitia uwekezaji katika miundombinu ya kubiashara na ujenzi wa viwanda; huo kumbuka ni Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu kuna maeneo maalumu ya uwekezaji ya Mkoa wa Kigoma. Lengo kuu la mradi ni kuwa na eneo maalumu wa uwekezaji llitakalokuwa na bandari huru (free port). Kutakuwa na mitaa ya viwanda, kongani za kitalii na kituo cha biashara. Hili limetengwa kutumia vizuri fursa za kijiografia ambayo itaweza kuhudumia nchi za Kongo, Burundi, Rwanda na Zambia. Kumbuka ni Mkoa gani huo? Ni Kigoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna eneo la uwekezaji Mkoa wa Mtwara eneo hili pia kutakuwa na uwekezaji jumla ya hekta 110 ambazo zimetengwa maalum kwa lengo la kujenga bandari huru ambapo kuna kampuni ambazo zinaendelea kufanya utafiti katika eneo lile na vilevile watajenga viwanda, Mkoa wa Mtwara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tano ni Mkoa wa Ruvuma, kuna uwekezaji wa jumla ya hekta 2030 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vikubwa (heavy industries) vitakavyotumia malighafi ya gesi na chuma. Viwanda vya kuongeza thamani na mazao ya kilimo kama korosho na viwanda vya vito vinatoka Mtwara hii ni Mikoa mitano Pwani, Dar es Salaam, Kigoma Mtwara na Ruvuma hii Mikoa yote inatoka Kanda ya Ziwa? Mikoa inatoka Chato? Tusipotoshe wananchi wetu, Watanzania wana akili sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna vipaumbele kwa mwaka wa fedha 2018/2019. Miradi mikubwa ambayo naona inasemwana sana, mradi wa Stiegler’s Gorge naona umekuwa ni mjadala mkubwa. Hata hivyo hiki ni chanzo cha nishati ya umeme. Tumesema Tanzania ya viwanda bila umeme hatuwezi kuwa na viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile kuna reli. Nakumbuka mimi katika Bunge la mwaka 2005 mpaka 2010 kulikuwa na mjadala wa Bunge kuhusu reli, barabara zinaharibika magari makubwa yanatumia barabara kila mwaka kuna fedha za kutengeneza barabara. Sasa sisi tunashauri Serikali inatekeleza, imekuwa kazi! Shirika la ndege… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)