Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Na mimi nashukuru kuweza kupata nafasi hii adhimu ya kuchangia kwenye Mpango huu wa mwelekeo wa mwaka 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiangalia mpango katika nchi hii lazima uwe na vyanzo ambavyo vitawezesha utekelezaji, lakini vile vile utawezesha upatikanaji wa mapto ya nchi hii; lakini vile vile utaonesha taswira ya mabadiliko ya maendeleo. Mimi sina tatizo na mipango iliyokuwemo kwenye masuala ya miundombinu, iko vizuri na tunakwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mpango mkubwa ambao unatazamiwa uweze kuleta mabadiliko chanya katika nchi yetu ni wa uanzishwaji wa viwanda mbalimbali, na hasa hivi ambavyo vimetangazwa na Waheshimiwa Mawaziri katika kila mkoa. Navyo vimejikita kwenye uzalishaji wa kilimo na mazao mbalimbali ambayo tunategemea tuweze kuyachakata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepitia hivi vitabu vyote viwili, mwelekeo na mpango wenyewe uliopo bado kama nchi hatujaonesha mwelekeo thabiti kwenye uzalishaji wetu ukoje. Hakuna projections sahihi ambazo tunalenga kwamba mwaka huu tutaweza kuzalisha mazao kiasi fulani. Kwa baadhi ya mambo tayari tumeshatoa maelekezo na ushauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, tulikuja tukaishauri hapa Wizara ya Kilimo na Serikali ijikite kwenye uanzishaji wa mbegu mpya za pamba. Leo mikoa ya Kusini tumetoa maelekezo na tunatarajia kama kweli wataweza kufanikisha ule mpango tuliokuwa tumewapa wa uzalishaji wa hekta zile zilizokuwa zimeshatengwa, tutaweza kupata mpaka marobota kwenye 600,000; kitu ambacho kwa uzalishaji uliokuwepo nyuma kilikuwa ni ndoto. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tukija kwenye upande wa mazao ya mahindi, bado Serikali haijaweza kusaidia katika eneo hili. Mahindi kwetu ndicho chanzo kikuu cha kila kitu; chakula na viwanda ambavyo vimo ndani ya maeneo yetu. Lakini leo bado nchi haijaweza, kuanzia kwenye mbegu tu ambazo tungeweza kuwapa wakulima wetu wakazalisha katika kiwango ambacho kinastahili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, takiwimu za kitafi zinaonesha kuwa asilimia 75 ya wakulima Tanzania waliozalisha mazao mbalimbali wanazalisha chini ya asilimia 30 ya mazao ambayo wangetarajia kuyapata ya asilimia 100. Nina maana gani? Maana yangu ni kwamba kwamba kila wakulima 100 kama ingeweza kuzalisha gunia 40; kwa eka moja mkulima huyu uwezo wake anazalisha gunia 12. Sasa hapa bado hatujajipanga, wakulima wanatumia nguvu zaidi mbegu bora haipatikani, mbolea bora haipatikani lakini vile vile na pembejeo za viuatilifu hazipatikani kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatakiwa ijipange itie msukumu zaidi kwenye uzalishaji wa mbegu bora, kwenye uzalishaji wa kuhakikisha kwamba tunazalisha mbolea katika nchi yetu. Lakini vilevile Serikali iweze kuhakikisha kwamba viwanda vile vya viuatilifu vilivyokuwa vimeanzishwa hapa nchini vizalishe viuatilifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kubwa zaidi nchi inatakiwa iweze kuwa na maono, kuwe na teknoloji ambayo ndiyo itaweza kututoa katika uzalishaji mdogo kwenda kwenye uzalishaji mkubwa hatimaye kupata bidhaa au raw materials kwa ajili ya viwanda tunavyotaria kuvianzisha. Tuna uzalishaji mkubwa wa chai katika maeneo yetu lakini ndani ya masoko ya nje Tanzania ni nchi ambayo inazalisha kidogo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii chai sisi tunazalisha kati ya tani 35,000 lakini wenzetu Kenya wao wako kwenye tani zaidi ya 400,000, lakini hizo 400,000 Tanzania sisi tunachangia kuwapa Kenya bidhaa. Mimi niipongeze Wizara ya Kilimo kwa uwamuzi thabiti wa kuanzisha mnada wa chai ndani ya nchi, na hii itawasidia sana Watanzania kile kidogo cha pesa za nje zinazopatikana ziweze kutumika ndani ya nchi. Ile chai iliyopo maeneo ya Iringa, Mbeya, Njombe na maeneo mengine kule Arusha na sehemu nyingine itaweza kusaidia sasa kuanzisha soko la minada ya chai kama tunavyofanya kwenye minada ya kahawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vivyo hivyo kama nchi tutaweza kuwashawishi wenzetu wa Malawi, Waburundi Warwanda kuunga katika huu mnada ambao tuliokuwa nao hapa hivyo kuhakikisha kwamba tunapandisha bei ya chai kutoka shilingi 600 kwenda kwenye 1000 na zaidi. Wito wangu ni kwamba Serikali ijikite kwenye vile vyanzo ambavyo tutaweza kuongeza mapato zaidi kuliko kuangali kwenye mambo ya miundombinu tu peke yake. (Makofi)

Kuhusu mifugo, Tanzania tunazaidi ya ng’ombe milioni 28 lakini kwa kweli katika uzalishaji wa maziwa hatumo kwenye ramani ya uzalishaji wa maziwa; tunazalisha watani wa lita milioni mbili tu ambazo vile vile hazina takwimu sahihi. Lakini Tanzania nchi moja ambayo inaagiza maziwa mpaka kutoka Zimbabwe, hii kwa kweli ni aibu. Kitu gani tunachoweza kushindwa kukifanya ndani ya nchi hii kuweza kukauka maziwa na kutengeneza maziwa ya unga? Tukichukua hao indigenous breed tuliokuwa nao hatoi lita moja moja tu kwa ng’ombe milioni nane , lita milioni…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)