Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na mimi naomba niweze kuchangia mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote na mimi naomba niungane na Watanzania wenzangu kutoa pole kwa Ndugu yangu Tundu Lissu kwa yale ambayo yalimkuta na nitoe pole na niseme tu kwamba hata niliposikia jana kuna baadhi ya Wabunge wenzetu wachahe wanaanza kuleta vijembe kwenye suala kama hili kwa kweli liliniumiza sana. Lakini niseme tu kwamba siku zote matatizo hayana itikadi na matatizo yanaweza kumkuta mtu yeyote yule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niingie kwenye Mapendekezo ya Mpango, tunafahamu wote kwamba kwenye hili kablasha tuliopewa na ndugu hapa Dkt. Mpango ukweli ni kwamba amezungumza vitu vingi sana kuhusu viwanda, kilimo na mambo mengine, lakini hatuwezi kupata viwanda bila kujali kilimo. Wenzangu wamezungumza mengi sana na jana niwapongeze waliotangulia kuzungumza kuhusu kilimo, lakini ukweli unapozungumza habari ya viwanda huwezi kuacha kilimo na ukakiweka pembeni, historia inaonesha nchi zote ambazo leo zina viwanda, nchi kama China na nchi nyingine nyingi ambazo leo zimeendelea ni kwa sababu walifanya mapinduzi katika kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Tanzania tunafahamu kwamba tunapotaka kufika mwaka 2020/2025 tunasema kwamba nataka Serikali hii iwe angalau wananchi wake wale na uchumi wa kati, uchumi ambao utaendeshwa kwa kutegemea viwanda. Lakini ukweli je, ni kwa sasa? Kwa sababu kwa muda huu ukiangalia kama lengo ni kupata malighafi kwa mfano kwenye viwanda vyetu ni kweli lazima tuangalie kilimo, lakini kwa sasa hali ilivyo wananchi wetu wamezalisha sana na wanalia kila kona hawana masoko ya mazao yao na viwanda vya kuweza kuwa-accomodate hayo mazao, kuweza kusindika mazao hayo hazipo. Kwenye hili tumebugi sana na hili niweze kusema kwamba tumerudi nyuma na wanachi wetu wanateseka sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wakulima wote waliolima tumbaku wanalia, wanalia wote waliolima mahindi na hivi ninavyozungumza Kanda za Nyanda za Juu Kusini katika Mkoa wa Songwe, Mkoa Mbeya, Mkoa wa Rukwa, Mkoa wa Ruvuma na mikoa mingine wanalia sana, mahindi yamekaa ndani, hakuna ayenunua yale mahindi, hivyo viwanda mlivyosemakwamba tupate malighafi kwa ajili ya kusindika mazao yetu tuonyesheni basi viwanda hivyo wakulima wetu wakauze mazao hayo kwenye hivyo viwanda basi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ni mbaya kwelikweli amezungumza vizuri ndugu yangu jana mmoja, leo mkulima anayelima ananunua mbolea bei kubwa, anakodi shamba bei kubwa, ananunua mbegu bei kubwa, lakini mwisho wa siku tunakuja kumfungia mipaka eti asiuze mahindi nje ya nchi lakini pa kuuza wakati huo Serikali haitoonyeshi tukauze wapi. Dhambi hii ambayo inatendwa na Serikali yetu na viongozi wa Chama cha Mapinduzi lazima niwe muwazi hapa jambo hili kama hamuwezi mkajadili kwenye caucus zenu mnajadili mambo mengine wananchi wetu msimu wa kulima ndio huu hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili ni baya sana na mwaka 2019/2020 hili jambo litawaghalimu na mjiandae kuondoka, kwaheri Chama cha Mapinduzi kwa sababu suala hili wameshindwa kujadili mambo ya msingi, wanajadili mambo mengine wanaacha suala hili la wakulima wetu. Mimi niseme kwamba leo tunazungumza 60% ya chakula kinachozalishwa nchini kinatoka Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, mkulima huyo hawezi kununua mbolea bila kuuza mahindi, hawezi kusomesha watoto bila kuuza mahindi, hawezi kufanya jambo lolote lile bila kuuza mahindi, leo wakulima hawa wanalalamika mimi naamini hasira hizi na machozi haya mwaka 2019/2020 wajiandae hao waliosababisha na Serikali hii na Chama cha Mapinduzi wala sio Serikali ya CHADEMA, wala sio ya CUF. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninajua wako wakulima pia wa tumbaku wanalalamika, wako wakulima wa mbaazi wanalalamika, wakulima wa korosho wenyewe wanasema bei imekuwa nzuri, lakini kiukweli bado hata wa korosho hao pia wamekopwa, bado hawajalipwa. Kiukweli kabisa tusipokuwa makini kwenye suala la kilimo mimi naamni kabisa Watanzania wengi watarudi nyuma kwasababu kilimo ndo kinaajiri 70% na kuendelea ya Watanzania walio wengi.

Naomba nizungumzie jambo lingine linalohusu utawala bora. Leo tumezungumza kuhusu utawala bora lakini ukweli ni kwamba viongozi wengi wanaotuhumiwa na rushwa kama ma-DC leo wanapandishwa vyeo wanakuwa Wakuu wa Mikoa. Hivi unawezaje kumpandisha cheo mtu ambaye alikuwa DC unampa Ukuu wa Mkoa anathumiwa kwa rushwa na ushahidi upo, TAKUKURU wameenda wamnachunguza kila kitu, kila mtu ameona kabla TAKUKURU hawatoa majibu leo Rais anaenda kumpa DC kuwa Mkuu wa Mkoa anayetuhumiwa kwa rushwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa hakuna utawala bora na hapa hali ni mbaya kweli kweli kama tutakuwa tuna- promote wanaoharibu nchi yetu, kwa kweli najua kabisa kwamba utawala bora, dhana ya utawala bora tuiondoe kabisa kwenye awamu hii ya tano. Lakini leo tunafahamu wote wanapozungumzia utawala bora tunafahamu misingi ya utawala bora ni pamoja na uwazi, leo Ndugu yangu Mpango hapo tumeambiwa Serkali imeokota vichwa vya treni pale Dar es Salaam bandarini, hivi ni kweli Serikali haijui ni kwamba vile vichwa vya treni vimetoka wapi. Uwazi uko wapi kwenye utawala bora lazima kuna uwazi, uwazi uko wapi, halafu vile vichwa vya treni vinajulikana vimeandikwa kabisa na majina. Sasa haya mambo leo Serikali inataka kununua vile vichwa vya treni, inanunua kutoka kwa nani inafanya biashara na nani, ni suala ambalo lazima tujue kabisa kwamba utawala bora ni tatizo ni janga kubwa nana na Dkt. Mpango ulichokizungumza kwenye ile kablasha kuhusu utawala bora, umezungumza tu kidogo tu mahakama sijui kujenga kufanya nini vitu vingi sana vya msingi ilitakiwa tuwaeleze Watanzania vinakaa vipi. Kwa hiyo kiukweli kwenye hili ni tatizo kubwa sana.