Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia Mapendekezo ya Mpango. Kwanza kabisa, namshukuru sana Mheshimiwa Rais wangu kwa kutuhudumia Watanzania kwa upendo, kwa kweli ni chaguo la Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili nirudi sasa kwenye Mpango nimeona wameongelea suala la afya. Kwenye suala la afya niishauri Serikali yangu, Serikali ya Chama cha Mapinduzi iangalie sana hospitali nyingi na hasa hospitali za rufaa ambazo hazijakwisha huko vijijini kwetu, wilayani na kwenye mikoa mingine kwa ujumla ili kuboresha huduma ya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Hospitali ya Rufaa ya Kwangwa ya Mkoa wa Mara imekuwa ikisuasua kwa muda mrefu sana. Hospitali ya Kwangwa imekuwa ikijengwa tangu sijazaliwa mpaka leo inaendelea kujengwa, pesa yake inakuja kwa matone matone kama ya mvua. Kwa hiyo, niiombe sana Serikali yangu iangalie sana suala la afya na kuangalia pia jinsi ya kuboresha zile hospitali zetu ndogondogo za wilaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika Mpango nimeona wameongelea kuhusiana na suala la maji, niiombe sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi iangalie sana hili suala la maji. Kama tulivyoomba Wabunge wengi na hasa Wabunge wanawake suala la kumtua mwanamke ndoo kichwani basi Serikali yetu katika Mpango huu ujao iangalie sana suala la maji kwa upana wake ili kusudi kumtua ndoo mwanamke kichwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika Mpango wameongelea mambo ya Serikali kwa ujumla kwa mfano kuna Mahakama, magereza na vitu vingine. Sijui kwa mikoa mingine kwa Mkoa wangu wa Mara kuhusiana na suala la Mahakama kwa kweli kumekuwa kuna shida sana na hasa vijijini.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, Wilaya ya Rorya kuna pesa ilishatolewa kwa ajili ya Mahakama lakini hadi sasa Mahakama haijajengwa hivyo kumekuwa na msongamano mkubwa katika Mahakama iliyopo Wilaya ya Tarime na kusababisha usumbufu na pia kuwasababisha wananchi wengi kushindwa kuhudhuria kutokana na umbali na kipato cha kwenda kule au nauli inakuwa ni ngumu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala pia la magereza, magereza zimejengwa muda mrefu sana toka kipindi cha Mwalimu Nyerere. Hivyo tuangalie suala la magereza katika Mpango huu kwa nchi nzima kutokana na ongezeko la watu. Kwa mfano, Wilaya ya Tarime watu kipindi hicho walikuwa wachache sana lakini siku hizi kwa kweli watu ni wengi sana na tunazaliana kwa speed ya hatari, kwa hiyo magereza ya Wilaya ya Tarime kwa kweli hayatoshi kabisa watu wanabanana sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine niongelee suala la madini. Humu kwenye Mpango wameongelea suala la madini na sheria zake na mambo mengine. Katika madini tunaiomba Serikali au mimi Mbunge wa Mkoa wa Mara naishauri Serikali iangalie sana suala la kulipa fidia kwa wananchi ambao wanakuwa wamechukuliwa maeneo yao na wawekezaji waliowekeza katika maeneo husika.

Mheshimiwa Spika,Kwa mfano, Mgodi wetu wa North Mara umechukua maeneo ya wananchi kwa muda mrefu sana kwa kweli, watu walikufa, wengine hawana pa kuishi mpaka sasa, wengine ni wazazi wetu, wengine ndugu zetu lakini hawana pa kuishi. Hivyo, niiombe Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi ifuatilie suala hili ili kuweka kwenye Mpango kuwalipa wananchi hao wa mgodini malipo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naongea haya kwa sababu nimemuona Mbunge wangu wa Tarime ambako ndiyo huko Nyamongo, Mheshimiwa Heche, yeye anawashwawashwa na uwanja wa ndege ulioko kwa Mheshimiwa Rais, anashindwa kuwaombea wananchi wetu walipwe fidia zao. Sasa yeye anatakiwa ajue kwamba wale wananchi wanahitaji yeye awatetee siyo awashwewashwe na mikoa mingine kitendo ambacho kwa kweli siyo kizuri sana na ni kitendo ambacho hakikubaliki hata kidogo kwa sababu yeye alitaka uwanja wa ndege uende nyumbani kwake? Au ni kosa Mheshimiwa wetu Rais kuzaliwa eneo ambalo uwanja wa ndege umepelekwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwanza kutokana na Mpango hili suala nina imani kabisa limeangaliwa kwa undani zaidi, kwanza kurekebisha au kubana matumizi. Kubana vipi matumizi basi na wanananchi wetu wanapaswa walisike hili. Ule uwanja ungepelekwa Shinyanga inamaanisha kwamba wananchi wangebomolewa nyumba, kwa hiyo ili kubana bajeti kule kulikuwa na maeneo ya wazi ni kwa nini uwanja usijengwe?

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, mambo mengine tunapaswa na sisi kupeleka siasa mitaani siyo tulete siasa Bungeni. Kwa hiyo, niwaombe sana Wabunge wenzangu mambo mengine yanapokuwa ya heri tufurahie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nishukuru sana, sina zaidi ila nasema Mbunge wangu Heche asiwashwewashwe, awatetee wananchi wa Nyamongo. Ahsante.