Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. RHODA E. KUMCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwanza nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu pia nitoe pole kwa familia ya Mheshimiwa Tundu Lissu huko aliko Mungu amponye kwa haraka ili arudi katika majukumu yake ya Kitaifa. Pia nitoe shukurani kwa Mheshimiwa Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Mbowe kwa kazi ya kujenga Taifa hili, pia namna anavyotetea na kujenga demokrasia katika Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia maendeleo ya uchumi wa Taifa hatuwezi kuacha kuongelea demokrasia ya nchi hii. Hatuwezi kuzungumzia uchumi wa Taifa hili bila kuzungumzia demokrasia na maendeleo katika Taifa hili, haiwezekani leo hii wafanyabiashara wakubwa,
wachumi mbalimbali wanatoa takwimu namna gani wanatoa taarifa ili Taifa hili liweze kwenda mbele, wanatoa taarifa na kuisaidia Serikali, wanatoa taarifa ambazo kimsingi zingeweza kulisogeza Taifa hili mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii watu wakipambana, wakitoa taarifa, wakikosoa Serikali, wanakwenda kupata shida na misukosuko mingi katika biashara zao na wengine wamefukuzwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi sasa kwenye hoja za msingi. Nataka nizungumzie kidogo namna gani ya kuboresha mikakati ya kuimarisha ukusanyaji wa mapato pamoja na kuzuia matumizi mabaya ya fedha katika taasisi za Umma. Tumekuwa tukipitia taarifa nyingi katika mashirika mablimbali ikiwepo TPA pamoja na Bandari; mifumo ya ukusanyaji wa kodi, mifumo ya namna gani wanatunza taarifa za fedha imekuwa ni kizungumkuti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka nimwambie tu mwalimu wangu Mheshimiwa Dkt. Ashantu Kijaji, kwamba tukishindwa kuboresha mifumo hii ya ukusanyaji wa fedha, namna gani ya kusimamia matumizi ya fedha katika taasisi hizi. Tunakwenda kupoteza fedha nyingi na leo hii tukiendelea kutoa taarifa hizi tutaonekana wabaya, tutaonekana tunaongea sana lakini lengo hasa ni kuhakikisha tunatoa taarifa ambazo zitaisaidia Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa napitia taarifa kuhusiana na masuala ya matumizi ya EFD mashine. Imekuwa ni kero, unakuta mfanyabiashara wa mahindi anatoka Mkoa wa Katavi anakuja kuuza mahindi yake Dar es Salaam mpaka afike Dar es Salaam ameshakutana na vizuizi vingi, lakini upatikanaji wa hizi mashine hizi electronic mashine imekuwa ni mtihani . Mfanyabiashara anatoka Wilaya ya Mlela anakuja mpaka Mpanda kutafuta tu hiyo risiti ili aweze kusafirisha mzigo wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ningemwomba Mheshimiwa Waziri katika suala zima la kuboresha hii mifumo ya namna gani ya ukusanyaji kodi, tuachane na mfumo wa kutumia manually kwa sababu watumishi wengi bila kuwasimamia vizuri unakuta tunapoteza mapato katika halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba tu kupitia mpango huu ambao kimsingi sijaona kwamba kuna sehemu imeandikwa kwamba mtakwenda kuhakikisha kila maeneo kila point ambayo itakuwa na ukusanyaji wa mapato mwongeze hizo mashine lakini kumekuwa na kero kubwa kwa hawa matrafiki. Sisi ambao tunasafiri kutoka Dar es Salaam mpaka Katavi unakutana na trafiki anakwambia umetembea over speed, ume-overtake lakini ukimwambia sasa okay nilipe Sh.30,000/= niendelee na safari yangu anakwambia sina mashine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini anakwandikia karatasi fekifeki tu unapita haijulikani hizo pesa zinakwenda wapi, leo tunapiga kelele watu wanakufa na njaa, watu wana shida ya maji, leo hii mngeweka mifumo hii mizuri na hizi mashine zikawepo za kutosha, pia kusimamia hii mifumo ya EFD kwamba kila center wanaposimama hawa matrafiki basi kuwe kuna hizi mashine ili kuondokana na huu udanganyifu ambao upo katika taasisi zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna masuala ya procurement entity, kumekuwa na udanganyifu mkubwa, tumekuwa tukipitia taarifa katika taasisi mbalimbali unakuta masuala ya documentation imekuwa ni issue imekuwa ni tatizo, unamuuliza procurement officer kwamba ni kwa nini kwenye masuala ya procurement masuala ya uingizaji wa bidhaa na utoaji wa bidhaa unakuta hakuna document ambayo inaonesha kwamba amepokea bidhaa kiasi gani na ametoa bidhaa kiasi gani, lakini unauliza unaambiwa kwamba mimi sina utaalam, tunakwenda kutengeneza Taifa gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu katika maeneo ambayo nafahamu kwamba tunapoteza vifaa vingi, tunapoteza pesa nyingi ni katika masuala ya procurement entity especially katika ofisi zetu ambao kuna Department za Procurement. Kwa kuwa kuna shida nyingine unakuta katika taasisi katika ofisi unakuta hakuna kitengo cha procurement ni mtu tu hata kama ni mhasibu anaamua tu kwamba leo sasa na-issue, natoa, nanunua, naagiza vitu natengeneza tenda, hatuwezi kwenda hivi bila kuboresha mifumo hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia watendaji wetu katika hii procurement entity wanatakiwa wasimamie, pia uhifadhi wa documentation katika hizo strong room wanatakiwa wapewe, ili leo tunapotaka kumwajibisha mtu tujue kabisa tunaanzia wapi. Watumishi wengi wamekuwa wanashughulikiwa wengine wanafukuzwa kazi kwa kosa hili tu, kutokuwa na documents za kimsingi ambazo wangeweza kuonesha na akajitetea, pia kumekuwa na shida katika masuala yaku-handleover ofisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unamuuliza Procurement Officer katika hizi taasisi zetu unamuuliza kwamba inakuwaje umepokea documents za ofisi bila kuoneshwa kwenye hiyo store umeacha vitu gani. Unamuuliza Procurement Officer anakwambia kwamba mimi nimepokea tu na kukabidhiwa ofisi, haiwezekani na ukiomba taarifa ya vifaa ambavyo vinakuwepo katika store hizi unakuta kwamba hakuna taarifa za ukweli. Sasa leo hii tunakwenda kusimamia vifaa, mali za umma pamoja na pesa za wananchi tunakosa taarifa kupitia kwenye masuala ya procurement, tutaendelea kupata shida, tutaendelea kupiga kelele huku wananchi wetu wakipata shida huku wachache wakijinufaisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije katika suala la viwanda. Mkoa wa Katavi katika bajeti iliyopita na pia katika mpango huu sijaona mkakati wa kuhakikisha mnatuongezea viwanda katika mkoa wa katavi. Hii ni tatizo, bajeti iliyopita wanatuambia kwamba tunaletewa viwanda zaidi ya nane, viwanda zaidi ya nane vitatusaidia nini Mkoa wa Katavi. Watanzania walioko kule wanahitaji viwanda zaidi ya hivi ambavyo wametupatia, kwa sababu na ukisoma kwa taarifa wanakwambia tumepewa viwanda nane na kiwanda kimoja kina uwezo wa kuajiri watu watatu, sasa hizo ajira ndio hivyo viwanda vya matamko ambavyo mnavisema , hatuwezi kuendeleza viwanda katika nchi hii bila kuwa na takwimu za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mapinduzi ya viwanda hayawezi kwenda tofauti na upatikanaji wa maji ya kutosha pamoja na umeme. Mkoa wa Katavi tuna visima vya maji zaidi 1000, leo hii watu wa Katavi wanakosa maji safi na salama kwenye mpango huu naona tu mikoa tofauti na Katavi sijaona kwamba kuna mkakati wa kuhakikisha Katavi tunapata maji. Hivi viwanda vya miujiza mnavyovisema kwamba tunahitaji kuingia kwenye mapinduzi ya viwanda ni vipi? Kwa sababu ninavyoelewa tunaposema mapinduzi ya viwanda lazima kuwe kuna upatikanaji wa maji wa kutosha pamoja na umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo katika masuala ya umeme wanatuletea majenereta mawili, tena majenereta mawili ambayo yamechoka. Nilitegemea kwamba kwa kuwa Serikali hii ni sikivu basi wangeongeza hata miundominu ya umeme kama masuala ya umeme wa REA lakini wametuletea umeme wa REA katika Wilaya ya Mlele, kitu ambacho hata watu wa Wilaya ya Mlele wameshindwa kulipia gharama, gharama zimekuwa kubwa lakini leo tungejikita kuhakikisha tunaweka miundominu katika mabonde yetu ambayo tuko nayo Mkoa wa Katavi leo hii tusingekuwa tunalalamika masuala ya umeme. Watu wa Mkoa wa Katavi, watu wa Wilaya ya Mpanda wanakaa wiki nzima hawapati maji, lakini bili zinakuja wananchi wanalipa, wanaletewa bili watu wana maisha magumu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia taarifa za TANESCO zimekuwa kizungumkuti. Umeme unakuja wanawasha, wanazima, watu wanaunguziwa vifaa vyao kwenye ofisi zao, hatuwezi kuendelea kulea uozo huu ambao unaendelea kwenye Mkoa wa Katavi bila kusema namna gani wanaitenga Katavi lakini namna gani wamekuwa wakitenga bajeti ambayo haijitoshelezi hususani katika masuala ya miundominu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna masuala pia ya umeme leo wametutengea zaidi ya bilioni mbili katika mradi wa maji ambao unatoka Kanoge mpaka kuja katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda. Ukisoma kwenye taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo ya Mkoa wa Katavi, wanasema kwamba umefika kwenye hatua ya ulazaji wa mabomba, sasa kwa muda wote huo kweli, watu wanakosa maji, watu wanakunywa maji ya kwenye mito, wanapata hata homa za maini, wanapata typhoid kupitia maji machafu ambayo wanakunywa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natamani ungefika Mkoa wa Katavi ukaona namna gani watu wa Katavi wanapata shida, lakini leo hii wamekuwa wanaitelekeza Katavi,watu wanakunywa maji machafu hawaleti pesa kwa wakati. Pia hii yote ni kutokana na kwamba wananchi wengi wamekuwa na uwoga wanashindwa kuhoji wakihofia hawa watu wasiojulikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie masuala ya mikopo kwa wanafunzi. Waliahidi kwamba watatoa ajira Rais alipokuwa Moshi tarehe moja hiyo siku ya Meimosi aliahidi kwamba ataajiri watumishi wapya lakini matokeo yake wamefanya replacement. Watu wengi walioonewa katika masuala ya vyeti feki au mwingiliano wa vyeti mara mbili, mfano katika shule ambayo ipo katika Wilaya ya Mpanda kuna Walimu ambao walihamishwa kutoka halmashauri moja kutoka Halmashauri ya Nsimbo kuja katika Halmashauri ya Mpanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu hawa katika mfumo wakajikuta kwamba majina yao yame-appear mara mbili leo mpaka hivi ninavyoongea hawajapata mishahara yao, lakini Serikali imekaa kimya, tumepiga kelele za kutosha na Waziri pia nimeshamweleza kuhusiana na tatizo hili lakini leo Serikali imekaa kimya. Sasa ni halali kweli kwa watu ambao wamesoma na wana vyeti mnawasulubu na kuwapa mateso makubwa haya, huku mkimwacha Bashite akila good time pale Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nizungumzie kuhusiana na suala la maliasili pamoja na hifadhi. Imekuwa pia ni tabia kwenye hii Serikali ya CCM kuendelea kutumia askari wa wanyamapori hususani katika Wilaya ya Mpanda, Jimbo la Mpanda vijijini Kata ya Isengule Paparamsenga, ni kwa nini Serikali hii ya CCM inashindwa kutenga maeneo au inashindwa kupima maeneo kwa wakati? Leo hii kwa kufeli kwa Serikali hii kwamba wameshindwa kupima maeneo hayo kwa wakati pia kuonesha mipaka ya hifadhi ni ipi na makazi ya wananchi ni yapi, matokeo yake wamekuwa wanawaacha wananchi wanachomewa nyumba zao, wanauliwa na askari wa wanyamapori lakini inafikia wakati mpaka wananchi wanabakwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni Serikali gani ambayo inawaagiza wananchi badala ya kwenda kuwaondoa na kuwapa elimu wananchi kuhusiana na suala la mipaka leo wanakwenda kuwabaka, wanawachomea nyumba zao ni Serikali gani hii ya CCM?