Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba (Intergovernmental Agreement – IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamuhuri ya Uganda kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (East Africa Crude Oil Pipeline – EACOP) kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania)

Hon. Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba (Intergovernmental Agreement – IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamuhuri ya Uganda kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (East Africa Crude Oil Pipeline – EACOP) kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania)

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia katika hoja iliyopo mbele yetu inayohusiana na bomba la mafuta kutoka Uganda mpaka Tanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kila jambo huwa linakuwa na mapingamizi, lakini tuseme tu kweli kwamba kwa kazi hii aliyoifanya Mheshimiwa Rais ya kuhakikisha kwamba bomba hili tunaweza kupewa huu mradi ni kazi ambayo anastahili kupongezwa sana, kwasababu kwanza ni mradi ambao umechukua muda mfupi sana, lakini wote tunafahamu ni kwa kiasi gani wenzetu wa Kenya walivyokuwa wanautaka mradi huu kwa udi na uvumba, lakini imekuwa bahati nzuri tuimeweza kuupata.

Mheshimiwa Naibu Spika, yako manufaa ya wazi wazi ambayo yatatokana na mradi huu maana hili bomba litakapojengwa maana yake ni kwamba hata barabara katika maeneo hayo yote zitapita na watu wetu ambao wako katika maeneo hayo watafaidika zaidi katika biashara zao mbalimbali, watafaidika na ajira ambazo zitatokana na mradi huu. Hii ikiwa ni pamoja na Serikali itaendelea kupata kodi katika mradi huu, lakini na ile tozo ya upitishaji wa mafuta kwa sababu lile bomba linalopita katika nchi yetu, kwamba tuta-charge kile kitu kinaitwa throughput ambayo kwetu sisi vilevile tutafadika nayo mbali na kodi mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niseme tu kwamba katika hili bomba linaliopita kama ingewezekana, maana nimeambiwa kwamba bomba hili tunalijenga sisi, Serikali ya Uganda pamoja na Kampuni za mafuta ikiwemo Total. Basi kama tungeweza ni vizuri na sisi nasi kama Serikali tungeongeza nguvu zaidi au mtaji mkubwa ilio kwenye lile gawiwo tutakalokuwa tunapata basi tuweze kupata kiasi kikubwa zaidi kuliko ambacho tunachoweza kupata kwa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba, jambo lingine ambalo limenifurahisha ni pale ambapo Serikai iliamua kuweka nafasi kubwa ambayo itapitisha bomba la gesi, ikiwezekana na miundombinu mingine labda bomba la mafuta ghafi lakini ikiwezekana na bomba la gesi

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niseme, kama inawezekana hebu Serikali ione uwezekano wa kupitisha bomba la mafuta kutoka Tanga litakalokwenda sambamba mpaka kule Uganda. Hilo bomba kama endepo litakuwepo vilevile litakuwa na manufaa makubwa. Kwanza, kama ni gharama za fidia tutakuwa tumeshalipa kwa hiyo tayari eneo tutakuwa nalo. Hata hivyo leo itoshe tu kusema kwamba wenzetu majirani mafuta yanafika Mombasa lakini wanaweza kuuza Uganda, Rwanda, Burundi na hata DRC kushinda sisi siyo kwa sababu nyingine, ni kwa sababu wana bomba la mafuta linalotoka Mombasa mpaka Kisumu; Mombasa mpaka Eldoret.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa sababu na sisi nafasi hii tumeipata, ukweli wa ni kwamba ukiweka bomba kutoka Tanga la mafuta likaenda mpaka Uganda maana yake sisi tutakuwa tumeshaminya zaidi ya kilometa 400, tutakuwa tuna kilometa 400 chini ya wao. Kwa hiyo tafsiri yake ni kwamba gaharama za mafuta kufika kwenye hizo nchi zitakuwa ni ndogo kwahiyo vilevile tutaendelea kufaidika zaidi kuliko wao kwa hiyo, hiyo kwetu itakuwa competitive advantage kama nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nitahadharishe tu juu faida ambayo tunayo lakini hatuiangalii sana, kwamba sambamba na hili bomba la mafuta gahfi tulilonalo tunayo miradi kama hii. Kwa mfano liko bomba hili la TAZAMA ambalo linatoka Dar es salaam mpaka kwa wenzetu kule Zambia pale Kapirimposhi na Ndola.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hili bomba hatulitumii sana, ni bomba la mafuta ghafi pamoja na mafuta masafi, lakini cha ajabu ni kwamba tunaacha kutumia lile bomba lakini malori mengi yanapitisha mafuta kupeleka huko na mtokeo yake ni kwamba kwanza yanaendelea kuharibu barabara lakini na gharama za uendeshaji nazo zinakuwa kubwa. Kwa hiyo, ni vizuri tukaangalia namna tunavyoweza kutumia hii miundombinu ambayo kwangu mimi ninaamini kabisa kwamba tukiitumia vizuri inaweza ikatuletea faida zaidi; ukilinganisha kwamba kwa Tanzania kijiografia tumekaa vizuri, kwamba inatupa nafasi nzuri zaidi ya kufanya biashara na wenzetu wanaotuzunguka kuliko wenztu ambao wako pembezoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo bada ya kusema hayo, na mimi naunagana na wenzangu kwa kuipongeza Serikali kwa kazi hii ambayo wameifanya kwa haraka, lakini niseme tu kwamba naunga mkono hoja. Ahsante sana.