Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la maeneo ya mipaka lipo katika maeneo mengi hasa mipaka ya Mbulu na Iramba; Manyara na Karatu; na Mbulu na Hanang. Tunaomba wapimaji waje kutatua na kusoma (GN) ili wananchi wajue wanapotakiwa kuwajibika kimaendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la mgogoro wa ardhi Yayeda Chini na mwekezaji aliyepora eneo la wananchi bila kupewa na Serikali ekari 3903. Mara nyingi Serikali hukubali kutoa eneo kwa wingi wa wananchi kusema apewe, lakini Wahadzabe, Wabarbaig mara nyingi jamii hizi hazijapewa elimu kuhusu ardhi, hivyo panapotokea mtu mmoja kuwadanganya wanaweza kutoa eneo hilo na baadaye mgogoro hautakwisha. Sasa kwa kuwa Wahadzabe ambao mara nyingi wana hamahama kutafuta matunda na asali pia wanahitaji ardhi hiyo na kwa bahati mbaya wapo wachache katika jamii. Ushauri wangu ni kwamba, wakati mwingine haki ya wachache izingatiwe ili jamii isipate tabu.