Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nianze kwa kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kuniwezesha kuwa na afya njema na kushiriki katika Mkutano huu wa Saba wa Bunge la Bajeti. Nampongeza Mheshimiwa Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson; Wenyeviti wa Bunge, Katibu wa Bunge Dkt. Kashililah , pamoja na watendaji wote wa Bunge kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake; Makamu wa Rais, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan; Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kasim Majaliwa pamoja na Baraza lote la Mawaziri, kwa kazi kubwa wanayofanya katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana tena sana Mheshimiwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi; Naibu Waziri, Mheshimiwa Angelina Mabula pamoja na watendaji wote wa Wizara kwa kazi kubwa na nzuri sana ya kuendelea kutatua migogoro ya ardhi katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na ziara aliyoifanya Naibu Waziri Mheshimiwa Angelina Mabula katika Mkoa wa Iringa na kutatua mgogoro uliokuwepo kati ya Manispaa na wananchi waliopo kwa maeneo waliyonunua kwenye Serikali ya Kijiji cha Igumbilo, Kata ya Igumbilo. Nashukuru sana mgogoro uliokuwepo unaelekea kumalizika kwa maelekezo sahihi aliyoyatoa au kuagiza Manispaa itekeleze, wananchi wamepatiwa viwanja katika maeneo yao, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mheshimiwa Angelina Mabula. Ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wetu wa Iringa unaendelea kupanuka kwa majengo pamoja na idadi ya watu kuongeza bado ujenzi holela nao unaongezeka, nimwombe Mheshimiwa Waziri, Ndugu yangu Lukuvi atusaidie kupunguza eneo la mipaka ya Manispaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa kuzirudisha nyumba za National Housing Serikali Kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.