Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ENG. STELA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nampongeza kaka yangu Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi, Waziri; na Naibu wake Mheshimiwa Angelina Mabula kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu ni moja tu kwa Mheshimiwa Waziri. Nyasa ni Wilaya changa, lakini ina potential nyingi hasa beach. Tunaomba msaada wa ruzuku ya upimaji wa ardhi ili kuipanga Wilaya yetu vizuri. Gharama za kodi za ardhi ni kubwa hasa kwa taasisi za Serikali ambazo zimehitaji maeneo makubwa na ulipaji wa ardhi hizo ni Serikali yenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini maeneo ya Serikali kama Vyuo mfano (UDOM), Sokoine na Vyuo vingine kama FDCs ambavyo maeneo hayo ni muhimu kwa ajili ya shughuli za vitendo kwa nini yasimilikishwe na kupewa hati kwa gharama za upimaji tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri alifikirie hilo kwa niaba ya ombi la Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na nawasilisha.