Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na kuwapongeza, Waziri Mheshimiwa Lukuvi, Naibu Waziri Mheshimiwa Angelina Mabula, Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara kwa kuleta bajeti hapa Bungeni ili tuijadili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Migogoro ya Ardhi, niipongeze Wizara na Waziri mwenye dhamana ya Wizara hii kwa kuendelea kutatua migogoro mingi nchini ikiwemo ya wakulima na wafugaji. Ni kwa nini Serikali isingetenge maeneo ya wafugaji peke yake na yakaainishwa na yakawekewa miundombinu kwa ajili ya kuwezesha wafugaji kutohama hama?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo ipo migogoro inayowahusu Maafisa Ardhi katika Halmashauri zetu. Tunashukuru hata hivi Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wanafanya juhudi kubwa sana kuwasaidia wanyonge waliokuwa wakipokonywa ardhi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wanagawiwa ardhi ya eneo moja zaidi ya watu wawili na kusababisha usumbufu mkubwa sana, lakini huwa tunapata tabu sana, Afisa anayeharibu Halmashauri moja badala ya kubadilisha anahamishiwa eneo lingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa Wataalam wa Ardhi; Halmashauri zetu nyingi nchini bado zina upungufu mkubwa na kunasababisha wananchi wengi kupata usumbufu mkubwa wanapotaka kupimiwa ardhi au kupata hati na sasa hivi na hili la vyeti feki nalo limechangia kwa kiasi kikubwa sana kuendelea kuwa na idadi ndogo ya wafanyakazi. Ni vizuri Serikali ikaweka utaratibu wa kujua nafasi hizi mapema ili kusaidia utendaji katika Halmashauri zetu na kupunguza kero kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mipango Miji, ni kwa nini miji yetu mingi haijapangwa, je kazi ya Maafisa Mipango Miji ni nini? Kumekuwa na mwingiliano mkubwa sana wa shughuli katika miji yetu kama vile hakuna wataalam. Ushauri wangu ni vizuri Maafisa Mipango Miji wangekuwa wanasimamia ile michoro iliyopangwa au kama miji haujapangwa basi wasigawe viwanja kabla ya kupitishwa michoro. Hata hivyo, kuna maeneo ambayo hayajapimwa ungekuwepo utaratibu maalum ili kuweza kusaidia jamii, kwa sababu kuna baadhi ya maeneo hayafikiwi kihuduma, wananchi wamekuwa wakipata mateso makubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu NHC, niipongeze Serikali kwa ajili ya kazi nzuri inayofanywa na Shirika hili, lakini tuombe majengo haya yajengwe hata katika miji midogo sababu hata wafanyakazi wanapata shida sana wanapohamishiwa mikoani. Ni kwa nini Halmashauri zetu zisitenge maeneo na kuingia ubia nao ili iweze kusaidia upungufu uliopo katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, haya mashirika yanayojenga nyumba kwa ajili ya Walimu kama Watumishi Housing nao wangefika katika Halmashauri zilizopo pembezoni ambako kuna matatizo makubwa sana ya nyumba za watumishi wakiwemo Walimu hata kama ya
kawaida sana ya vyumba vitatu au viwili ili kuyafanya maeneo hayo pia wafanyakazi waweze kuishi kama mijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, malalamiko ya ukarabati wa nyumba za mjini, naomba kujua je kuna sheria yoyote iliyotolewa na Serikali nyumba za kati kati ya mji zisikarabatiwe zijengwe maghorofa. Sababu kunakuwa na malalamiko kwa wananchi wa Manispaa ya Iringa kutopatiwa vibali vya kukarabati nyumba zao hata kama ni magofu na kusababisha majengo mengi kuwa na hali mbaya sana. Sababu hawana uwezo wa kujenga maghorofa sasa tunaomba Serikali itupatie ushauri. Sasa hivi hakuna wawekezaji kabisa kutokana na hali ya uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.