Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Napenda kujibu baadhi ya hoja ambazo zimejitokeza kutoka kwa Kambi ya Upinzani na baadhi ya wachangiaji wa upande wa kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya kwanza wanasema kwamba Serikali imeiweka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kijeshi, kimabavu na kwa kukiuka Katiba.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja hii naomba niigawe katika makundi mawili. Kuna hii dhana potofu ambayo imekuwa ikizungumzwa kwamba Serikali imepeleka maaskari wengi wakati wa uchaguzi Zanzibar, dhana ambayo siyo sahihi.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema siyo sahihi kwa sababu gani? Kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi, mfano mdogo tu najaribu kutoa kwamba katika kila kituo cha uchaguzi inahitajika angalau wakae askari wawili na Zanzibar kuna vituo vya uchaguzi zaidi ya 1500. Kwa hiyo, ukichukua kwa kituo askari wawili maana yake unahitaji askari 3,000 na kati ya askari 5,000 walioko Zanzibar unabakiza askari 1,500 ambao hao hao wanahitajika kwa ajili ya mambo ya vital installation pamoja na misako, doria, kukaa standby, kufanya upelelezi na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nashangaa uchaguzi ambao umefanyika tarehe 25 Oktoba upande wa Tanzania Bara kwa mfano tumetumia askari mpaka wa Zima Moto, JKT kwa sababu askari tuliokuwa nao hawatoshi. Takwimu zinaonyesha polisi mmoja anahudumia wastani wa wananchi 1,200. Kwa hiyo, kimsingi hili jambo linajaribu tu kuenezwa vibaya na hasa ukizingatia yale matishio ambayo yalikuwa yakienezwa ikiwemo ulipuaji wa mabomu, jitihada za kuchoma nyumba moto, kulikuwa kuna kila sababu ya Serikali kuwa makini sana katika kuhakikisha kwamba uchaguzi ule unakwenda kwa salama na amani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala ambalo linazungumzwa kwamba Katiba imekiukwa...
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya kumwambia Mheshimiwa Rais Magufuli aingilie maamuzi ya ZEC na hoja ya kwamba vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo viko kwenye Muungano kutekeleza jukumu la kikatiba kusimamia usalama wa raia na mali zake, hapo lipi ni kuvunja Katiba? Ni kumwambia Rais aingilie mamlaka ya ZEC ama polisi kuchukua kazi yake ya msingi ya kulinda raia na mali zao?
kuhakikisha kwamba uchaguzi wa marudio Zanzibar umekwenda kwa hali ya usalama na amani na Zanzibar na Tanzania kwa ujumla sasa hivi watu wanaishi vizuri, kwa salama na amani na watu wanafanya shughuli zao kama kawaida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo, kuna hoja ambazo zimezungumzwa kwamba kuna watu wamekamatwakamatwa hovyo na sijui kuna watu wanaitwa mazombi, tumezungumza hapa kwenye Bunge kwamba sisi hatuwatambuwi. Tulichokisema na ambacho tunakirudia kusema hapa sasa hivi ni kwamba vyombo vya ulinzi vitatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa taratibu. Matukio ambayo yameripotiwa na ripoti hii ambayo inazungumzia matukio mengi sana ya uvunjifu wa Sheria za Uchaguzi yaliyosababisha Tume ikatoa maamuzi hayo na sisi tulichunguza. Kwa mfano, tulichunguza suala la kuzidi kwa kura ukilinganisha na wapiga kura, tumewabaini watu na ushahidi upo waliofanya matukio hayo.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la watu kuzuiliwa kupiga kura, watu Mawakala wa Vyama vya Siasa wamebururwa kama mbwa njiani, tumewabaini na tumewakamata, hakuna mtu aliyeripoti habari ya mazombi.
MBUNGE FULANI: Toa ushahidi.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Kuna suala la kufutwa kwa namba za matokeo kwenye fomu kwa makusudi kabisa, tumewabaini wahusika na wamekamatwa. Kuna takiribani watu zaidi ya 149 tumemaliza uchunguzi wao sasa uko kwa DPP, ni kazi ya DPP kuamua kuwapeleka mahakamani, sisi tumeshafanya kazi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo mengi yamefanyika ya ovyo kabisa katika uchaguzi halafu leo mtu anakuja hapa anasimama anasema uchaguzi ule.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tumesema kwa mamlaka yetu tuhamishe vituo vya kuhesabia kura. Kuna vituo na majina naweza nikawatajia hapa, kituo kimoja kimetolewa Wawi kimepelekwa Chenjamjawiri, kweli si kweli? Akatae pale Mbunge Wawi, akatae!
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nataka niseme jambo moja kwamba suala la ulinzi na usalama katika nchi hii halina mjadala au mbadala. Leo hii nimesikia baadhi ya Wabunge wa upande wa kule wanataka kuleta vitisho. Mimi nataka nichukue fursa hii niseme hapa hapa Bungeni kwamba tunatoa onyo kali, kama wewe unaamua kutumia Bunge hili kuchochea vurugu hakuna mtu ambaye yuko juu ya sheria. Wale viongozi mnasema wamekamatwa iwe kiongozi wa chama chochote au raia, ikiwa wamekiuka sheria za nchi hii watakamatwa na watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tu niseme kwamba jukumu hilo ndiyo jukumu la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani na Jeshi la Polisi kuhakikisha kwamba tunasimamia usalama wa nchi hii. Niwapongeze sana Jeshi la Polisi kwa kazi nzuri sana waliyoifanya NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Kuna mtu anaitwa Pinde sijui ambaye ndiye alikuwa Msimamizi wa Uchaguzi amekiri mwenyewe kabisa kwamba alisimamia kinyume na sheria za uchaguzi. Sheria za Uchaguzi zinasema kura zihesabiwe kwenye kituo leo kiongozi ambaye amepewa mamlaka ya kusimamia uchaguzi Pemba anahalalisha uvunjifu wa sheria halafu sisi tusichungeze leo mnasema uchaguzi siyo huru na haki!
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nasema kwamba watu wote walioshikiliwa kwa kukiuka taratibu za uchaguzi kwa masuala ya jinai, polisi imeshafanya uchunguzi imeshaupeleka kwa DPP. Ni wajibu wa DPP, mahakama na mamlaka nyingine kuchukua hatua zinazostahili, sisi tumeshamaliza kazi yetu. Katika hilo hatutamstahi mtu yeyote iwe Mbunge, iwe mwanachama wa kawaida, iwe viongozi wa chama chochote anayekiuka sheria za nchi hii, sheria itafuata mkondo wake.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.