Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuzungumza juu ya mgogoro wa muda mrefu wa shamba la Malonje. Serikali inatakiwa kumaliza mgogoro huu ambao Serikali imekuwa ikipiga danadana kila siku. Hakuna jambo linaloweza kushinda Serikali kwani tunashuhudia jinsi Mheshimiwa Waziri Lukuvi anavyojitahidi kutatua migogoro mbalimbali katika nchi hii na mara ya mwisho aliwaahidi wananchi wa Vijiji vinavyozunguka shamba hilo kuwa atakuwa Waziri wa mwisho kuzungumzia mgogoro huo. Hivyo wananchi walishajenga imani kubwa sana kwake kwa kauli aliyoitoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamwomba aumalize mgogoro huu. Kama kuna makosa yaliyofanywa na viongozi wa Wilaya, Mkoa ndiyo maana yote hayo yamefikishwa kwake hakuna sababu tena ya kukwepa jambo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wa Tarafa ya Kipeta na hifadhi ya akiba ya Uwanda Game Reserve. Tunaomba mipaka ichunguzwe upya kwani uwekaji wa mipaka ya hifadhi hiyo imeingilia maeneo ya Vijiji jambo linalofanya wananchi wa maeneo hayo kukosa ardhi ya kilimo na mifugo, tunaomba Serikali ifuatilie jambo hili haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa vijiji hivyo wapo hapa Dodoma kutaka kuonana na Mheshimiwa Waziri Lukuvi, pia ikishindikana kumwona Mheshimiwa Waziri, wamwone Mheshimiwa Rais. Tunaomba wasikilizwe (ni juu ya shamba la Malonje).

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.