Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mikakati mingi mizuri ya Wizara ya Ardhi, bado kuna changamoto nyingi katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti hii ungewekwa mkakati wa dharura wa kuhakikisha inawapimia mapema kabla hawajajenga wawe na hati ili kuondoa migogoro ya fidia kupunjwa na kunyanyasa wanaopisha ujenzi wa miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya ardhi Manispaa ya Mpanda; Kata nyingi za Manispaa ya Mpanda hawajapimiwa je, ni lini sasa Wizara kupitia Ofisi za Kanda itaharakisha kupima maeneo haya ili wananchi wapate hati ambazo zinaweza kuwasaidia kukopa fedha katika benki. Kata ya Ilembo, Misunkumilo, Kata ya Kakese, Kata ya Mwamkulu na Kata ya Kashamili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara isisubiri watu wajenge nyumba zao nzuri halafu inakuja kubomoa na kuwalipa fidia ndogo na za kucheleweshwa. Katika Bajeti hii Mheshimiwa Waziri ameonesha wazi kuwa na dhamira ya kutatua kero ya fidia kwa kuanzisha Bodi ya Fidia hii ikasimamiwa vizuri itasaidia vizuri na kuondoa kero za malalamiko nchini, hii nadhani ipangiwe mkakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi na wananchi wa Kata za Mpanda hotel na Misunkumilo; naomba bajeti hii ione namna ya kutatua mgogoro huu ni wa muda mrefu sana .

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupunguza gharama za uuzaji nyumba za NHC Manispaa ya Mpanda; mpaka sasa hakuna faida iliyopatikana kutokana na uuzaji wa nyumba hizi, je hamwoni kuendelea kuziacha nyumba, kama gharama haziwezi kupungua basi zipangishwe kwa watumishi wa Serikali kwa sababu kuna uhaba wa nyumba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miundombinu katika nyumba hizo bado haitoshi, barabara, hospitali, shule, masoko. Hivyo kwa kuzingatia ukosefu wa miundombinu hii ndio inasababisha watu kushindwa kuhamia kule.