Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mgogoro wa ardhi ya vijiji-Kakonko; Vijiji vya Nyakayenzi na Kiga vina mgogoro wa mpaka wa muda mrefu kwenye bonde la Mto Ruhwiti. Mgogoro huo ulipelekea Kijiji cha Kiga kuhodhi ardhi ya Nyakayenzi kwenye mpaka wa vijiji hivyo. Mheshimiwa Waziri alipokuja Kigoma, akiwa Kibondo viongozi wa Nyakayenzi walifanikiwa kuonana na kuongea na Waziri aliagiza DC ashughulikie kutatua mgogoro huo ambao maamuzi aliyotoa hayakuwaridhisha wananchi wa Kijiji cha Nyakayenzi maana wananchi wa Kiga walipewa haki ya mashamba kwenye eneo la Nyakayenzi. Wananchi wa Nyakayenzi walitaka mashamba hayo yaendelee kutambuliwa kama ya Nyakayenzi huku yakilimwa na wananchi wa Kiga kwa mujibu wa ramani na mipaka ya vijiji hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, walikata rufaa kwa Waziri Bunge lililopita na kuwasilisha kwa Naibu Waziri wa Ardhi. Ushauri, naomba Serikali/Wizara isimamie na kumaliza mgogoro huo kwa kujibu au kushughulikia rufaa hiyo. Bado wananchi wa Nyakayenzi wana imani na Wizara kuwa haki itatendeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro wa ardhi kambi ya JKT Kanembwa na Vijiji; kumekuwepo na mgogoro kati ya eneo la Kambi ya JKT Kanembwa na Kijiji cha Kazilemihunda kwani mipaka imekuwa ikibadilika mara kwa mara kwa Kambi kuongezea eneo na kuingia katika ardhi ya Kijiji cha Kazilamihunda. Ushauri, maeneo hayo yapimwe kwa kushirikisha Serikali ya Kijiji cha Kazilamihunda na uongozi wa Kambi ya Kanembwa JKT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ardhi ya wananchi iliyochukuliwa Kambi ya Wakimbizi-Mtendeli. Kuna wananchi wa Kasanda walionyang’anywa ardhi ili kupisha wakimbizi kwenye Kambi ya wakazi Mtendeli. Baada ya ardhi hiyo kuchukuliwa wananchi hawakupewa ardhi nyingine kwa matumizi ya kilimo na mifugo. Ushauri, wananchi hao wapewe ardhi nyingine pamoja na fidia kwa mazao yaliyoharibika hasa eneo la juu ya Kambi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri juu ya bomoa bomoa, kumekuwepo na bomoa bomoa ya nyumba zilizokwishajengwa hasa zile ambazo zimekamilika ama kwa kigezo cha nyumba, kujengwa eneo lisilostahili kama vile hifadhi ya barabara, open space, hifadhi ya Mto, Ziwa, Bahari, na kadhalika. Mjenzi anakuwa na documents zote za ardhi, kama vile ramani, kiwanja na amelipia na kadhalika. Ushauri, kwa nini ardhi wasisimamie kuhakikisha hawatoi kibali cha ujenzi bila kuwasiliana na Wizara ya Miundombinu na Mazingira kujiridhisha kuwa eneo hilo linaruhusiwa kujengwa nyumba kuliko kuacha ijengwe kisha inabomolewa.