Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Waziri kwa hotuba nzuri pamoja na watendaji wote wa Wizara kwa kazi inayoleta faraja kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri inayoendelea kufanywa yapo mambo yanayohitajika kufanyiwa kazi kuwa nguvu:-

- Wizara kuongeza speed ya kupima ardhi yote ya Taifa hili. Kiasi cha asilimia 15% ni kidogo sana, eneo kubwa bado halijapimwa.

- Kupima maeneo kwa ajili mifugo na malisho. Sheria ya Ardhi imeelekeza Waziri kutenga ardhi kwa ajili ya mifugo na malisho, kuyagazeti na kuyalinda.

- Serikali itueleze ni maeneo kiasi gani na wapi maeneo ya malisho yametengwa na kupimwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuongeza speed ya kuanzisha Mabaraza ya Ardhi katika Wilaya zote hapa nchini, ili kurahisisha usuluhishi wa migogoro ya ardhi. Mabaraza tuliyonayo ni 53 tu, yanayofanya kazi ni machache sana. Mabaraza haya yawezeshwe kifedha ili yaweze kutekeleza majukumu yao vizuri. Pia Serikali iwezeshe Wajumbe wa Mabaraza kwa kuwapa posho wanapokaa wafanye kazi yao vizuri. Serikali/Wizara kufanya follow-up kwa Maafisa Ardhi popote walipo watekeleze majukumu yao kwa kuwajibika na kuuza ardhi mara mbili (double allocation).

Mheshimiwa Mwenyekiti, Viongozi wa Vijiji wapewe elimu wafuate Sheria ya Ardhi katika kugawa ardhi ya wananchi. Viongozi wanakula rushwa wanauza maeneo makubwa bila kuitisha mikutano ya wananchi. Waziri atoe tamko hapa Bungeni lakini pia semina kwa viongozi wa Vijiji ni kiasi gani cha ardhi kinaweza kuuzwa na viongozi wa vijiji na kiasi gani hawaruhusiwi. Wafugaji wanapokelewa vijijini wanatoa fedha nyingi, wanapewa maeneo ya kufugia wakati wananchi wengine hawana habari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima kama Taifa tuwaze miaka 100 ijayo mbele. Leo tunajivunia Tanzania tuna ardhi kubwa, tusipopanga matumizi bora na hii ardhi tutakosa ardhi kwa matumizi muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mashirika na Taasisi zinazojenga majengo na nyumba za makazi wajenge nyumba kwenda juu (flats) na sio kwenda chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wawekezaji wa miradi mbalimbali wapewe ardhi kuendana na mradi wao au eneo linalofaa kwa mradi huo. Maeneo ya kilimo yabaki kwa kilimo, maeneo ya malisho yabaki kwa malisho na maeneo ya ujenzi yasiwe ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la uanzishwaji wa miji kiholela bila utaratibu; maeneo mengi kila leo miji mipya imeanzishwa kando kando ya barabara, hakuna maelekezo yoyote, hakuna udhibiti, hayo yanakuwa makazi holela.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Watumishi House waongeze speed ya kujenga nyumba za watumishi, speed yao ni ndogo sana. Wafike kwenye wilaya mpya ikiwepo Kaliua wajenge nyumba za watumishi kusaidia makazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba (National Housing) waliahidi kuja Halmashauri ya Kaliua kujenga nyumba tangu mwaka 2016. Napenda kujua ni lini watafika na maeneo tulishayatayarisha ya kutosha na yapo mjini.