Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabaraza ya Ardhi, nilichangia katika hotuba ya Utumishi na Utawala Bora, kwamba mabaraza haya tuyajengee uwezo japo hata kutembelewa na Mwanasheria as an observer ili tu kujionea proceedings kusudi upungufu
utakaobainika, itafutwe namna ya kuupunguza kwa kutumia ama semina au mafunzo ya muda mfupi kadri ya mazingira yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Diaspora vs Umiliki wa Ardhi; lililoko tamko ambalo limeleta mkanganyiko hasa kwa Watanzania ambao wanaishi nje ya nchi lakini wamebaki na utaifa/uraia wao kama Watanzania. Tafsiri ya watu wengi walioko nje ni kwamba kwa Mtanzania anayeishi nje hastahili kumiliki ardhi kumbe iwekwe wazi kwamba ni haki kwa Mtanzania kumiliki ardhi hata kama anaishi nje ilimradi tu ni raia wa Tanzania kwa wale waliobadilisha uraia diaspora per se, utaratibu mbele ya safari uje utazamwe ilimradi kufungua fursa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mafinga Mjini vs upimaji wa ardhi na uwepo wa Master Plan. Mji wa Mafinga unakua kwa kasi sana kutokana na biashara ya mazao ya misitu (mbao, nguzo, milunda na kadhalika.) Ukuaji huu umeleta mahitaji ya ardhi iliyopimwa kwa kasi, hata hivyo uwezo (capacity) wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga kuendana na speed hiyo umekuwa mdogo kutokana na uhaba wa watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi/ushauri, Wizara ifikirie kuwezesha upimaji/uandaaji wa Master Plan kwa Mji wa Mafinga na maeneo mengine ambayo ni miji ili kuepukana na ujenzi holela/squatters. Kwa jitihada zangu nilionana na Profesa Lupala ambaye kwa ushirikiano na ushauri wake, wanafunzi wa field wa Ardhi University watatusaidia kukusanya data ili baadaye Wizara kwa kushirikiana na Halmashauri yetu tutakamilisha Master Plan. Nimewasilisha ombi la kupewa baadhi ya watumishi wa ilivyokuwa CDA hasa Maafisa Ardhi, Mipango Miji na Wapimaji kama jitihada za kukabiliana na uhaba wa watumishi wa kada ya ardhi ili kufanikisha azma ya kupanga Mji wa Mafinga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi; naamini ni jambo la gharama kubwa lakini kama sehemu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kukabiliana na migogoro ya wakulima na wafugaji, hatuna namna zaidi ya Wizara hii ku-take lead kwenye suala hili ambalo linagusa kilimo, maliasili na hata usalama wa nchi. Tukifanikisha jambo hili tutaondokana na malalamiko mengi ya kila mmoja katika Taifa kuanzia kilimo, kufuga, hifadhi na hata uwekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutengwa maeneo ya Industrial Clusters; wakati tunapoelekea uchumi wa viwanda ni muhimu kila Halmashauri kutenga maeneo kwa ajili ya viwanda na kwa kuwa uwezo wa kupima maeneo yote ni mdogo, basi angalau tuanze na jambo hili kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji ambayo imekuwa ikilisema jambo hili mara kwa mara katika kulitekeleza. Nashauri utolewe Waraka kwa kushirikiana na TAMISEMI kuziagiza Halmashauri kutenga hizo Industrial clusters.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.