Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kukushukuru wewe kwa kunipa fursa hii ya kuchangia katika hotuba hii ya Waziri wa Ardhi. Pili, nampongeza Waziri pamoja na watendaji wake wote kwa mashirikiano yao yaliyopelekea kutayarisha hotuba hii na kuiwasilisha kwa utaalam mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangia hotuba hii napenda kuchangia maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Usimamizi wa Ardhi, hivi sasa nchi yetu inakabiliwa na ongezeko kubwa la watu. Watu kutoka nje ya nchi yetu wanafika nchini kuomba umiliki wa ardhi kwa matumizi mbalimbali. Hivyo, Serikali yetu ni lazima iendelee kuweka utaratibu mzuri wa ugawaji wa ardhi ili kuepuka kutoa fursa kwa wageni na kuwanyima wazawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya ardhi inaendelea kuongezeka siku hadi siku hasa kati ya wafugaji na wakulima. Hii inatokana na ongezeko kubwa la wafugaji na upungufu wa maeneo. Nashauri Serikali kuweka mpango maalum wa kutofautisha maeneo ya wafugaji na yale ya wakulima ili kuondosha migogoro hii ambayo inaendelea kupelekea watu wa makundi hayo kuuawa. Aidha, Serikali iweke kima maalum cha ufugaji kuwa na kima maalum cha wanyama ili kuepuka matatizo haya.