Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee Mabaraza ya Ardhi; mojawapo ya malengo ya kuanzisha mabaraza haya ni kupunguza migogoro ya ardhi katika maeneo mbalimbali hapa nchini na pia kuharakisha usuluhishi wa kesi za ardhi. Pamoja na malengo haya mazuri mabaraza haya haiwezekani kutekeleza majukumu yake, ufanisi umekuwa mdogo kwa kukosa vitendea kazi, watumishi wachache wenye maslahi duni na kutopelekewa fedha za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto kubwa zaidi ipo katika Mabaraza ya Kata ambapo ndipo kuna kesi nyingi na hawapatiwi fedha za kuendesha shughuli zao. Serikali kuwaachia Halmashauri wawezeshe mabaraza haya ni kuzidi kuyadumaza mabaraza haya kwani Halmashauri zenyewe vyanzo vyake ni vya kusuasua na wakati mwingine hazina fedha kabisa kwani mahitaji ni mengi zaidi ya fedha hizo za own source katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ifanye yafuatayo:-

Kwanza, kuyawezesha mabaraza ya Ardhi ya Wilaya ikiwa ni pamoja na kuongeza watumishi ili mabaraza haya yatimize majukumu yao kwa mujibu wa sheria; na

Pili, Wizara ichukue jukumu la kuyawezesha Mabaraza ya Kata kuliko kuziachia Halmashauri, kwani mapato ya Halmashauri hayatoshelezi. Sehemu ya fedha za kodi ya ardhi katika Wilaya husika kiasi fulani zibaki ili kuyawezesha Mabaraza ya Kata katika Wilaya husika.