Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kuipongeza Wizara na Mheshimiwa Waziri kwa juhudi wanazofanya katika kuyapatia ufumbuzi masuala ya migogoro ya ardhi nchini ikiwemo Monduli. Mheshimiwa Waziri anakumbuka mwaka jana 2016 Machi alipokuja Monduli alikabidhiwa mashamba 13 yaliyofutwa na Rais kwa ajili ya wananchi lakini mpaka sasa wananchi wamezuiwa kutumia ardhi pamoja na kwamba wao wameshapanga matumizi na kubainisha maeneo ya malisho na eneo la kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa masikitiko wamiliki wa awali waliyapeleka malalamiko kwa DC na DC kuzuia wananchi kutumia ardhi hiyo, mpaka itakapoenda tume ya kuchunguza kama mchakato wa kufutwa ulifuatwa. Masikitiko yetu ni kwamba Rais ameshafuta mashamba je, kuna mtu mwingine mwenye mamlaka zaidi ya Rais? Naomba kauli ya Mheshimiwa Waziri kuhusu mashamba ambayo Rais ameshayafuta lakini bado wananchi wananyimwa kuyatumia. Naomba Ofisi yake itoe waraka wa kuelekeza namna bora ambayo wananchi wanaruhusiwa kutumia ardhi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo Mheshimiwa Waziri alitoa agizo kuhusu Ndugu Olemilya Mollel aliyejichukulia ardhi kinyume na taratibu ambapo pia aliagiza yeye kuondoa walinzi wa jeshi wenye silaha wanaolinda ardhi yake ambayo ni pori tu, miti na majani, (agizo lake halikutekelezwa) badala yake wananchi sasa wanakamatwa na kutozwa hadi milioni moja kama faini na mwenye shamba (naomba kauli yake ili kunusuru wananchi).

Mheshimiwa Mwenyekiti, uanzishaji wa Baraza la Ardhi Wilaya ambapo sisi tumetoa jengo tayari. Tunaomba kupatiwa Afisa Ardhi Mteule. Tunaomba wananchi wapewe angalau miaka mitano ya kulipia nyumba za NHC.