Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii. Awali niipongeze sana Wizara hii kwa jitihada za kazi wanazozifanya ndani ya Wizara hii. Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri wake pamoja na wasaidizi wake wamefanya kazi nzuri sana. Tunawapongeza hasa kwa kutatua migogoro mingi ambayo kimsingi ilikuwa inawagusa sana wananchi. Tunawapongeza na kuomba tuwaombee heri sana waendelee kutenda haki na misingi iliyowekwa ya kisheria juu ya kuwasaidia wananchi hasa walalahoi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuzungumzia tatizo la migogoro ya ardhi ya vijiji vya Kabage, Sibwesa, Mkungwi, Kagunga na Kapanga vilivyoko kwenye Wilaya ya Mpanda. Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ina mgogoro wa muda mrefu sana wa vijiji hivi, tunaomba sana Mheshimiwa Waziri apange ziara aje amalize tatizo hili, akishirkiana na Wizara ya Maliasili. Wananchi wengi wanataabika hawana ardhi ya kufanyia kazi wakati ni vijiji halali ambavyo kimsingi kama vitasimamiwa tatizo hili tutakuwa tumelipunguza na kuwafanya wananchi waendelee kufanya shughuli zao. Naomba sana Waziri husika aje atatue matatizo ya Mkoa wa Katavi hasa Wilaya hii ya Tanganyika iliyoko kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo ningependa kuzungumzia ni tatizo la kupata hati za kimila kwenye Wilaya ya Tanganyika. Karibu maeneo yote ya vijijini tuna tatizo kubwa sana la kukosa huduma ya kupata hati za kimila. Kuwasaidia wananchi hawa wanapopata hati za kimila tunawajengea uwezo wa kiuchumi, kwani watapima mashamba yao na watakuwa na nafasi ya kutumia dhamana ya hati miliki ili waweze kwenda kwenye taasisi za fedha, huduma hiyo kwetu sisi hatuna. Naomba Waziri aone kwamba ni wakati muafaka sasa kupeleka huduma hii kwenye maeneo yote ya nchi yetu hasa maeneo ya pembezoni kwenye Wilaya hasa zile ambazo ni changa. Tunahitaji huduma hii ili iweze kutatua matatizo yanayoikabili Wilaya kwa kukosa huduma ya hati miliki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo ningependa kuzungumzia ni uhaba wa wafanyakazi. Wataalam wa ardhi hasa Wilaya mpya, naamini na nchi nzima bado kuna tatizo kubwa sana. Tunaomba Mheshimiwa Waziri anapokuja aje na majibu sahihi yatakayosaidia kutoa
suluhisho hasa wataalam hawa ambao kimsingi wanahitajika ili waweze kufanya kazi ambazo zitawasaidia wananchi na kutatua migogoro mingi ambayo iko kwenye Halmashauri za Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo tunahitaji kupata vitendea kazi, wataalam ambao wapo hata huko kwenye Wilaya hawana vitendea kazi vya shughuli ya upimaji ambavyo ni pamoja na magari. Unakuta Halmashauri haina gari, haina vifaa ambavyo vinahitaji kwa shughuli za kupima hivyo viwanja, matokeo yake wanaenda kwa miguu kitu ambacho hawawezi kutekeleza na kwenda na kasi ambayo ipo. Tunaomba sana hasa kwenye Wilaya yangu tupate wale ambao wana uwezo wa kufanya hiyo kazi ili tuwasaidie Watanzania. Kimsingi tukitekeleza hili tutakuwa tumetoa kero kubwa ambayo inawakabili wananchi kwa kukosa huduma. Tukipata hao watalaam nina imani kwamba eneo zima la suala la ardhi na migogoro ambayo tunaizungumzia itapungua kwa kiwango kikubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na naunga mkono hoja.