Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. James Kinyasi Millya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Mwenyeiti, muda wa dakika tano ni mdogo sana nifanye mambo mawili, moja nimkaribishe sana Mheshimiwa Lukuvi Simanjiro, matatizo ya Simanjiro Wizara ina takwimu inaongoza Tanzania kwa kuporwa kwa ardhi yake, lakini la pili kwa sababu Wizara yako imesogezwa tarehe, wananchi walikuwa wapo tayari kuja kukuletea matatizo yao, ninaomba hata baada ya kupitisha bajeti yako wananchi wachache waje kukusalimia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo mwaka 2005 nilikuwa kijana peke yake wa Wilaya nzima aliye graduate degree ya kwanza, baada ya miaka mitatu baadae ndio mwingine mmoja anapatikana. Kwa nini ninasema hivyo, Wilaya ya Simanjiro imejaa watu wengi ambao hawajasoma, wale wachache wanaojua kuandika na kusoma waliopewa Tarafa; waliopewa kuwa Wenyeviti vya Vijiji wame-take advantage ya hali ile na kuwaumiza wananchi na kuwachukulia ardhi yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba Mheshimiwa Waziri fika Simanjiro hali ni mbaya kweli kweli, lakini niseme tu kitu kimoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mashamba makubwa, shamba namba 24 Lorbosoit ya aliyekuwa Katibu Tarafa ya Emboreet Mzee Brown ambaye bahati mbaya au nzuri ni Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya, amechukua heka 8,000 lakini kama haitoshi, baada ya kushindwa kulima na kufugia amebadilisha shamba lile anataka kufanya ni la wanyamapori na kuwauzia Wazungu. Ninaomba Mheshimiwa Waziri umetoa directives nakumbuka kama Waziri ulisema hakuna kubadilisha ardhi yoyote, kubadili matumizi yake bila idhini yako, huyo Mzee anafanya ujanja kutumia nafasi yake ya CCM kubadilisha mazingira hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna Muhindi mwingine Kata ya Loiborsiret, Kijiji cha Loiborsiret eneo la Motio, ameamua kuchukua ardhi kubwa ya wananchi kununua moja, moja heka mia, mia mbili lakini sheria zipo wazi, haiwezekani kijiji kikawa na uwezo wa kugawa zaidi ya heka 50 haiwezekani, Mheshimiwa Waziri nakuomba usaidie hilo. Kuna kijiji kingine cha Narakauwo mtu anaitwa Jerry Hoops amekuja ameingia kama mbia mwenzake na Mtanzania mmoja, alichukua heka 2,000, shamba lile lipimwe lina zaidi ya hekta 10,000 mpaka sasa hivi naomba uliingilie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Kilombero kuna zaidi ya mashamba 50,000, maelfu na maelfu ya hekari ambayo yamechukuliwa. Mheshimiwa Waziri tatizo hili hatuwezi kukusaidia kwa dakika hizi tano ninakuomba Mheshimiwa Waziri ninakukaribisha uje Simanjiro, umeenda Arumeru, umeenda Monduli, umeenda Babati naomba uje Simanjiro wanakusubiri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Naberera kuna Mwenyekiti wa Kijiji amekuwa ni mtu wa ajabu naomba uangalie, kwa kweli mimi kwa ufupi niongee kwenye hilo tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo pale Wizarani kwako una watu mahiri kweli, kuna mtu anaitwa Ndugu Lwena ninamfamu ni mwanasheria mahiri kweli hali rushwa ni mtu ambaye sijawahi kuona, nimeishi naye nimefanya naye kazi mwaka 2009, anaweza kukusaidia. Kuna kesi ya Lekengere, Faru Kamunyu and others versus Minister of Natural Resources and Tourism ya mwaka 2002, Mahakama ya Rufani ilisema huwezi ukachukua ardhi inayomilikiwa kimila bila kupata idhini ya Rais. Rais peke yake ndiye mwenye uwezo wa kufanya hivyo. Ukisoma pamoja na Sheria ya Land Acquisition Act ya mwaka 1967, pamoja na kuwapa wananchi fidia hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri naomba utusaidie Simanjiro imeoza, waliotutangulie wengine kwenye madaraka hayo hawajatumia vizuri, ninaomba tusahihishe historia, watu wangu wanaumia, ardhi inaumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nirudie kwenye suala la ardhi Mkoa wa Arusha kwa ujumla. Kuna watu walioletwa na Mwalimu Nyerere kwa nia njema ya kuwekeza, baada ya kumaliza uwekezaji na kuchukua ardhi yao, sasa wanayageuza mashamba yale kama mtaji. Inawezekanaje Mtanzania akanunua ardhi yake peke yake, sana Serikali muingile, kuna watu wakubwa wana mashamba makubwa pale Arusha, Arumeru na unafahamu. Mzungu anataka kwenda ulaya kwenda ku-retire kukaa kwenye nyumba ya wazee, anabadilisha ardhi yetu kama sehemu ya kiinua mgongo chake, badala ya ninyi kusimamia arudishiwe machinery na gharama ambazo ametumia kwenye shamba lile, anatuuzia mashamba yetu, NHC walinunua kule Kisongo, ninampongeza Ndugu Msechu ni kijana mzuri mwenzetu anafanya kazi kubwa ninaomba tembelea Angola.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamchanganya kama Serikali, hamjui kama mpo kwenye ubepari, hamjui mpo kwenye ujamaa you just confuse, philosophy mnaichanganya mpeni afanye biashara ili atakapopata faida aendelee kusaidia watu maskini wengine, lakini mnamchanganya ni mtu mzuri mwema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia Mungu awabariki sana.