Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wa Wizara kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanyia nchi yetu. Naomba nichangie kwa kifupi kama ifuatavyo:-

(i) Mabalozi wote wa Tanzania wawe chachu ya maendeleo ya nchi yetu hasa kwenye sekta ya viwanda na biashara ili tutimize azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Tanzania ya viwanda. Waweze ku-connect fursa za kiuchumi ili tupate malighafi ya viwanda vyetu kwa urahisi, lakini zaidi tupate soko la uhakika la nje la bidhaa za viwanda.

(ii) Mabalozi wetu waiuze Tanzania katika sekta ya utalii. Tanzania haifananishwi na nchi yoyote ya Kiafrika, tukiacha South Africa, kwa kuwa na mbuga nzuri za Ngorongoro, Serengeti, Mlima Kilimanjaro na kadhalika. Wanyama wazuri wawe kivutio cha watalii wengi kuja Tanzania ili tuinue uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.