Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nawapongeza Waziri na Naibu, pia watendaji wote katika Wizara kwa kazi nzuri na makini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kuchangia kuhusu makazi ya wakimbizi. Serikali ilipokea wakimbizi kutoka Burundi na kufufua makambi ya Katumba na Mishamo (Mpanda) na Ulyankulu (Tabora) na mwaka 2009 walianza kupewa uraia, lakini kwa sasa bado watu wachache hawajapata uraia. Wito kwa Serikali ni kuwataka Umoja wa Mataifa kufadhili maeneo hayo katika huduma za jamii mfano afya, elimu, barabara na uchumi kwa kuwa maeneo hayo yalikuwa yanafadhiliwa na UN. Hivyo ni muhimu nchi ambazo zimeathirika kwa namna moja au nyingine na kupokea wakimbizi basi UN izisaidie kama wanavyofanya kwa nchi zingine.

Tunaomba kauli ya Waziri ni lini Serikali itaibana UN kufadhili makazi ya Katumba (Mpanda - Katavi) kwani kwa sasa wametoa ambulance moja na kukarabati Kituo cha Afya Katumba, kituo ambacho bado hakitoshi kabisa kwa wananchi zaidi ya 60,000 waliopo Katumba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kuhusu huduma za Konseli Miji ya Biashara. Tunajua kwa Serikali imefungua Balozi nchi ambazo tunafanya nazo biashara lakini mfano China Ubalozi upo Beijing, lakini Mji wa Biashara ni Guangzhou ambao upo mbali sana toka Beijing. Kwa hiyo, ni muhimu kuwa na huduma za konseli kwa watu wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, nizungumzie suala zima la kuimarisha amani. Tunazidi kutoa wito kwa Wizara kuongeza juhudi za kuimarisha amani kwa nchi jirani za Burundi, Kongo, Rwanda na Uganda ili kupunguza kuingia kwa wakimbizi ambao wanaathari nyingi katika jamii yetu kiutamauni, kiuchumi, ujambazi, wizi wa nyara na silaha haramu. Hivyo, Tume zilizoundwa ziendelee kuimarishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, ni kuhusu Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kuna nyanja nne za ushirikiano katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Changamoto zilizopo katika maeneo mawili tunazikabili vipi na tunajiandaa vipi kwa maeneo ambayo bado kuingia katika ushirikiano? Vilevile Serikali iendeleze kushirikisha Wabunge wa EAC kama nchi katika kujenga hoja na kusimamia vema maslahi ya nchi. Nawasilisha.