Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kunijaalia afya njema na kuweza kuchangia Wizara hii. Pia nawatakia Watanzania Ramadhani Kareem. Naunga mkono hotuba/ maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kuchangia kwa kuipongeza Wizara kwa kupata hati safi za ukaguzi wa mahesabu kasoro Ofisi moja tu ya Ubalozi wa Tanzania nje ya nchi. Ni vema wakati Waziri akifanya winding up aitaje ofisi hiyo ni ya Ubalozi wa Tanzania iliyo katika nchi gani na hatua gani zimechukuliwa na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kutaka Serikali yetu kusaidia Watanzania wanaoishi na kufanya kazi nchi za nje (diasporas) kupata haki na stahili zao, kuondoa manyanyaso kwa Watanzania lakini pia wabaki na passport zao katika baadhi ya nchi ambazo Watanzania wananyang’anywa passport zao na Serikali za nchi hizo. Kwa ufahamu wangu passport ni document halali inayotakiwa kumilikiwa na raia wa nchi husika. Je, inakuwaje katika baadhi ya nchi duniani Watanzania wakiajiriwa wanaporwa passport zao na Serikali za nchi hizo wanazofanya kazi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu demokrasia na haki za binadamu, kufuatia uchaguzi wa Zanzibar wa tarehe 25 Oktoba, 2015 ambapo matokeo yake yalibatilishwa kimazingaombwe hali iliyopelekea uchaguzi ule kurudiwa na Chama cha CUF na vyama vingine vya mageuzi kuususia na kuleta sintofahamu kwa wananchi, taarifa za International Observers nazo ziliweka wazi kuwa mshindi katika Uchaguzi wa tarehe 25 Oktoba, 2015 alikuwa ni mgombea wa chama cha CUF, Mheshimiwa Maalim Seif Shariff Hamad.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sakata hili imepelekea Taasisi ya MCC (USA) imefunga ofisi zake na kusitisha kutoa shilingi trilioni 1.06. Je, fedha hizi shilingi trilioni 1.06 sawa na US$ milioni 472.8 zingeendesha miradi mingapi ya maendeleo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina ushauri kama ifuatavyo:-

(i) Waziri aeleze kuna mikakati gani ya kufanya mazungumzo ya kutatua jambo hili ili MCC irudishe ofisi dar es Salaam na tuweze kurejeshewa shilingi trilioni 1.06 ambayo ni sawa na US$ milioni 472.8.

(ii) Je, hatutafanya makosa ya kuwekewa vikwazo vya kiuchumi kimataifa kwa kukandamiza demokrasia? Naomba Waziri afafanue.

(iii) Serikali ianzishe utaratibu Watanzania wanaoishi nje na kufanya kazi (diasporas) waruhusiwe kupiga kura wakati wa Uchaguzi Mkuu kama zinavyofanya nchi nyingine duniani.

(iv) Kuna nchi tulizopewa viwanja, majengo na rasilimali nyingine na tumeshindwa kuvijenga (Oman na Mozambique) lakini pia katika ofisi 35 baadhi ya majengo yamechakaa sana, zifanyiwe ukarabati.

(v) Mabaharia wa Tanzania waliosomea katika Chuo cha Bandari - Temeke Dar es Salaam wanasumbuliwa kuwa vyeti vyao havitambuliki kimataifa. Serikali ichukue hatua zinazostahili ili vyeti vya chuo hiki vitambulike kimataifa.