Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na nchi yetu kuwa na mahusianao na nchi mbalimbali duniani kuna kila sababu ya kuboresha maeneo muhimu ili kudumisha mahusiano makubwa na yenye manufaa kwa nchi yetu ikiwemo yafuatayo:-

Kwanza, kuunganisha soko la ndani ya nchi yetu na masoko ya nje kwa kufanya uboreshaji wa mazao yanayozalishwa nchini, kuyapandisha thamani ili yaweze kutumika nchi nyingine ambazo tuna uhusiano mzuri na nchi yetu, kupata manufaa kwa kupitia masoko ya ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kupeleka wanadiplomasia wenye uwezo. Kutokana na mazingira halisi ya nchi yetu ni vema wanadiplomasia nafasi zao zikawa na faida kwa nchi yetu, kwa kutumia uwezo wao kuchukua mambo ya nchi nyingine na kuyaleta nchini kwetu yalete manufaa. Kuwa na utaratibu wa kuunganisha Watanzania wanaoishi nchi za nje kulingana na kauli mbiu ya Awamu ya Tano, kauli mbiu ni viwanda ni vema Wizara hii ya mambo ya nje kuangalia ni jinsi gani watasaidia Taifa kuendana na kauli mbiu ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni namna gani Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi kubeba ajenda ya utalii ili Taifa letu liweze kunufaika na watalii, endapo kama Wizara itaweza kutangaza na kubeba ajenda ya utalii ili kupata fedha za kigeni pamoja na kujenga uhusiano mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Watanzania wanaoajiriwa nje ya nchi hususan kazi za ndani, wamekuwa wakiuawa na kuteswa na kunyanyaswa ni vema Wizara ikawa na mipango endelevu ya kumaliza na kufuatilia kwa ukaribu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, usalama wa wanafunzi wanaosoma nje ya nchi ni mdogo sana, Wizara ni vema pamoja na Mabalozi waweze kuangalia kwa ukaribu wanafunzi wote na kuwapa misaada ambayo inaweza kuwa ndani ya uwezo wao.