Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru kwa kunipa nafasi. Moja ni suala la Ubalozi huko tuliko kwenye viwanja vyetu. Nikuombe Mheshimiwa Waziri, viwanja maeneo mazuri Nairobi; ukienda nyumba yetu pale London; ukienda Sweden; kote ninaamini tukiweka uwekezaji tutapata fedha za kuendesha Balozi zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa suala la kufungua Ubalozi na watu wa Israel na tumeona faida zake, sasa tumeanza kupata watu wanakuja kutalii kutoka Israel. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu, niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge, mimi kama mwanasiasa, ukiona mtu ambaye ni adui yako umefanya jambo akakusifia, ujue liko tatizo. Ukiona umefanya jambo adui yako akasema umekosea, maana yake umepatia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni Taifa. Nami naomba sana nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa aliyofanya. Niwambie Waheshimiwa Wabunge, naomba niwambie duniani kote, extractive industry inaenda kubadilika na atakayekuwa kwenye historia amebadilisha extractive industry ni Mheshimiwa Rais Magufuli. Leo duniani kote, kwenye kila mgodi mambo yatabadilika kwa sababu sasa ilikuwa ni vitu vinatengenezwa, mnaambiwa kuna tatizo, lakini sasa amefungua mlango. Nina hakika kila ambako kuna extractive industry, mambo yatabadilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwambieni Watanzania tusiogope. Kwenye hili lazima kama nchi tuwe nyuma ya Mheshimiwa Rais, tumuunge mkono aendelee. Ninayo hakika wawekezaji watakuja mezani. Wakati fulani ili watu waje mezani lazima na pa kuanzia. Kama ni suala la ku-negotiate, ume-negotiate toka mwaka 1999, hatujapata vya kutosha. Nadhani umefika wakati, hii ndiyo ilikuwa njia ya kuleta haya mabadiliko ambayo nina hakika tutayapata kama Taifa.

Mimi niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge, tumuunge mkono Mheshimiwa Rais, huu siyo wakati wa kutupiana maneno.

Ni wakati wa kufikiri. Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.