Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mimi nitakuwa na mambo machache sana. Mheshimiwa Waziri Balozi Mahiga wewe ni Waziri mzoefu nina uhakika yote yaliyosemwa utatuonyesha njia, namna ya kutoka hapa tulikofika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo mawili; katika hotuba yote hii, Mheshimiwa Balozi Mahiga hujaweka hata sentensi moja kuhusu wakimbizi (refugees). Katika Mkoa wa Kigoma tumekuwa na wakimbizi tangu miaka ya 1960 na nilidhani kupitia diplomasia yetu hii ya mahusiano na majirani zetu, ni wakati muafaka sasa kwamba wakimbizi hawa wangerudi kwao. Wewe unajua, Mkoa wa Kigoma una raia zaidi ya nusu milioni wanaotokea katika Jamhuri ya Congo, Burundi na Rwanda. Leo DRC mambo siyo mabaya sana Kusini mwa DRC, watu wao hawa wangeweza kwenda kuhifadhiwa katika DRC na makambi yakawa ndani ya DRC, hivyo hivyo kwa Burundi na Rwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kwa sababu muda wenyewe ni mdogo, nizungumzie juu ya huu mpango kabambe wa UN. Naomba unisikilize. Mpango kabambe wa UN wa kusaidia maeneo yaliyoathirika na ujio wa wakimbizi (Refugee Hosting Area Program). Wewe na Wizara yako na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi mna uwezo mkubwa mkakaa na hawa UNHCR mkaja na program ya kusaidia maeneo ambayo tumekaa na wakimbizi kwa miaka zaidi ya 60 in this country.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana muda wenyewe ni mdogo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natumaini kwamba mtatoa majibu yanayofaa.