Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Haji Khatib Kai

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Micheweni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. HAJI KHATIB KAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunirudishia dakika zangu tano kwa vile umetumia busara kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie pale ambapo nilibakiza. Nilisema ili kumaliza matatizo ambayo wavuvi wetu wamekuwa wakiyapata kule nchini Kenya, basi ni vyema Serikali hizi mbili zikarudi kwenye mkataba ambao Serikali hizi mbili Mawaziri wetu wa Mambo ya Nje walikubaliana na kusaini. Kwa hiyo, ninao hapa naomba Watendaji wachukue ili wampatie Mheshimiwa Waziri ili jambo hili liweze kumalizika kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati yetu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, mimi nikiwa mmoja ambaye niliteuliwa kwenda nchini Afrika Kusini, Pretoria, tulipofika Ubalozi tulipatiwa taarifa ya majengo nane ambayo tulienda kuyakagua. Katika jengo moja ambalo tulilikagua na kupewa taarifa yake ni jengo ambalo linamilikiwa na SMZ yaani Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jengo hili kunataka umakini mkubwa sana. Katika Serikali ya SMZ kuna chombo cha kutunga sheria kama vile Bunge la Jamhuri ya Muungano na katika Baraza la Wawakilishi ziko Kamati za Kisekta ambazo zimekuwa zikizungukia miradi na kuona miradi ambayo inamilikiwa na SMZ.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wasiwasi wangu hapa ni kwamba Mheshimiwa Waziri atutoe wasiwasi hapa wakati wa ku-wind up: Je, kuna utaratibu wowote au kuna makubaliano yoyote ya jengo hili ambalo linamilikiwa na SMZ ambalo sasa hivi linataka kuingizwa katika Jamhuri ya Muungano? Je, endapo litakuwa hivyo, hakuna maneno yoyote? Hakuna malalamiko yoyote ambayo yanaweza kuleta shida huko mbele?

Mheshimiwa Mwenyekiti, jengo la pili ambalo tulienda kulikagua ni jengo la Tanzania House ambayo ni Ofisi ya Ubalozi. Jengo hili unapoliangalia katika sura ya mbele utaliona ni zima, lakini ukweli ni kwamba jengo hili limeshafanya crack au nyufa. Jengo hili utashangaa kwamba nyumba ya Balozi na Maofisa ziko vizuri, ziko salama, lakini unapokuja katika jengo la Ofisi ya Ubalozi maisha ya Maafisa Ubalozi wetu tunayaweka rehani. Tusiombe litokee tetemeko la aina yoyote. Endapo kutatokea tetemeko la aina yoyote, basi tunaweza kupoteza Maafisa Ubalozi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jengo ambalo linakaliwa na Afisa Ubalozi wetu ambaye anaitwa Rose Jairo. Jengo hili kwa bahati mbaya sana na hali halisi ya nchi ya Afrika ya Kusini na usalama wa nchiā€¦