Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami kwa haraka haraka, napenda kukushukuru. Naishukuru Wizara na Watendaji wote kwa ujumla kwa mawasilisho ya bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku moja nateta na mwenzangu hapa, nikawa najiuliza kuna kila sababu sisi kama Bunge kwa nafasi yetu Kikatiba kuna mambo bila kujali itikadi lazima tuwe kitu kimoja kwa maslahi ya Taifa. Sasa hata kama uzalendo wako ni wa mashaka, kwenye suala hili la mchanga mimi matarajio yangu kuna mambo tunaweza tukabishana kwa kutafuta kiki na kadhalika, lakini kwenye masuala kama haya ya mchanga wa dhahabu my dear friends, brothers and sisters hili jambo ushauri wangu, nawaomba tuwe kitu kimoja, tuwe nyuma ya Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka tuwape mileage, mtu anazungumza eti atashitakiwa kwenye Mahakama za Kimataifa, si zipo! Kazi yake ni nini? Tutaenda, tutakutana huko. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu, Waheshimiwa Wabunge kuna mambo hebu tuweni kitu kimoja; tunaweza kujijengea huko nje kwa wananchi, ni aibu kubwa sana especially kwa jambo hili. Jambo hili hata mtu ambaye ni layman analiona kwamba ni jambo la thamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kuna Tume nyingine ambayo inafiti ni namna gani tumeibiwa sisi na kuhujumiwa kiuchumi katika suala la mchanga. Sitarajii kwamba suala hili tuwe against kwa mipango mizuri hii ya Serikali, kwa sababu tunalia maji, tunalia dawa, sasa tunalia majengo. Juzi tumesema zahanati hazijakamilika, tunalia hapa majengo huko Ubalozini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mambo kama haya tushirikiane kuunga mkono jitihada hizi. Nami ningetegemea hata ambao ni Wanasheria nguli wa nchi hii, sasa wajipange kwamba kama Serikali itapelekwa kwenye hizo mahakama wao watakuwa msitari wa mbele kushirikiana na Serikali kuhakikisha kwamba wanatetea maslahi ya Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe Waheshimiwa Wabunge kuna mambo hebu sisi tuwe united, tuwe kitu kimoja. Tusipinge tu simply because itikadi zipo tofauti. Haya ni mambo yanagusa maisha yetu, ni mambo yanagusa maisha ya vizazi vyetu. Kama kuna makosa yalifanyika, hatuwezi kukaa macho tukasema sasa tuache tuendelee tu kukosea, hiyo haiwezekani kwa sababu kulifanyika makosa. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu dakika pia ni chache, ningependa kuzungumzia pia umuhimu wa Wizara kuhakikisha kwamba inapeleka Maafisa katika Balozi zetu. Maafisa wapo wachache, kuna baadhi ya Balozi unakuta Balozi yupo mmoja, hana Afisa wa kumsaidia kufanya kazi na Balozi huyu ni mgeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.