Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kama Mjumbe wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, sikitiko langu ni sawasawa na Wajumbe waliopita. Tatizo la bajeti, Bunge tunapitisha lakini mwisho wa siku pesa haziendi kwa wakati kwenye kasma ambayo sisi tumeipelekea. Sasa Mheshimiwa Waziri utakapokuja kujibu hoja yako jioni, ninaomba utuambie safari hii utafanya nini kuhakikisha fedha hizo zinafika kwa wakati hasa zikasaidie kazi za Balozini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, tunazungumzia uchumi wa kidiplomasia. Sisi kama Kambi, Mbunge wetu ameelezea vizuri sana ni jinsi gani inabidi tujikite kwenye uchumi wa kidiplomasia. Na mimi nazidi kusisitiza kwamba bila kuwa na uchumi wa kidiplomasia hatuwezi kufanya vizuri kwenye zama hizi za maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeingia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, tunafahamu biashara nyingi sana zinaendelea, lakini kundi kubwa la wanawake ambao ndio wajasiriamali wakubwa, sijaona kama Wizara imefanya juhudi za makusudi kuweza kutambulisha fursa hizo za kijasiriamali kwa wanawake wa Tanzania kwa ujumla wake. Kuna maonesho mbalimbali yanafanyika, likiwemo Jua Kali na mengineyo, sijaona kama Wizara imetangaza hata kwa kutumia Televisheni ya Taifa kuwaeleza wanawake wa Tanzania kuzijua hizo fursa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ni ya muhimu sana. Tunajua kwamba Mabalozi wanalipwa mishahara kule waliko. Wanatumia juhudi gani kuitangaza Tanzania hasa katika maeneo ya kiutalii pamoja na mambo mengine ambayo watu wetu wanaweza wakanufaika na hizo nchi. Nadhani ifike wakati tupeleke wataalam na kama wapo, wapewe onyo kali wasipofanya kazi zao na wajibu wao wa kuitangaza nchi katika hizo nchi wanazokaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, tuna tatizo katika Wizara hii. Balozi mmoja, kwa mfano Balozi wa Msumbiji, anasimamia na Balozi nyingine zinazomzunguka. Ni kweli tunabana bajeti, lakini mwisho wa siku ufanisi unakuwa mdogo kwa sababu hakuna pesa zinazokwenda mahali pale. Kwa hiyo, nashauri bado ninafikiri tuna wasomi wengi katika Taifa hili, ninaomba wapewe nafasi za Ubalozi katika hizo nchi badala ya kutegemea Balozi mmoja kusimamia Balozi zote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie Chuo cha Diplomasia, Kurasini. Chuo kile ni cha muhimu sana na wote tunajua kwa nini kilianzishwa. Hivi tunavyoongea kile chuo wenzetu wa Msumbiji walijitoa, lakini pia hatuna pesa ya kukiendeleza kile chuo. Mapato yanayotumwa kwenye kile chuo ni madogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri atakapokuja tunaomba atuambie, tunasimamiaje chuo kile ili kiendelee kutoa Wanadiplomasia makini katika Taifa letu la Tanzania? Tunataka kujua kwa nini wenzetu wa Msumbiji walijitoa na wengineo? Basi watuachie tubadilishe matumizi ya chuo kile kiweze kusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie suala la Jumuiya ya Afrika Mashariki na lile jengo letu la AICC pale Arusha. Nataka kujua linasaidiaje? Kwa sababu ninaamini pesa zinazopelekwa bado ni ndogo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)