Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naomba tu Wizara ifuatilie sana ushauri alioutoa Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna Wizara sensitive kama Wizara ya Mambo ya Nje kwa sababu dunia ya leo imekuwa kijiji. Katika mambo yanayohusu biashara na uchumi wa kidiplomasia kati ya mataifa na mataifa, engagement ya Wizara ya Mambo ya Nje ni muhimu sana kwa ajili ya kutoa ushauri ni mambo gani yanatakiwa kufanyika? Hatua ya kulinda rasilimali za nchi hii ni mtu mwendawazimu anayeweza asipongeze; lakini namna gani unalinda rasilimali za nchi hii, inaweza ikaligharimu sana hili Taifa na kuliingiza kwenye consequences nyingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Taifa hili wote tunafahamu kwamba nchi hii ina mgogoro na Acacia Mining, mgogoro huo kwa sura ya kwanza unajenga hisia na sifa za kisiasa ndani ya nchi, lakini sura ya pili ya mgogoro huu unakwenda kabisa ku-demoralize spirit ya investors walioko nje kuja katika Taifa hili kufanya investment. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo tu Acacia, ukiangalia ardhi kwenye Wizara ya Mheshimiwa Lukuvi, imekuwa ni sifa kunyang’anya watu ardhi na imekuwa ni sifa kunyang’anya wawekezaji ardhi, jambo hili mbele ya safari litalifanya Taifa hili liende likawe kama Zimbabwe. Wakati Mugabe anaanza sera hii ya kunyang’anya watu mashamba, kuwakandamiza investors wa nje, alipigiwa makofi na wananchi wake kama ambavyo leo tunapigiwa makofi, lakini leo ninavyoongea kwenye Bunge hili, Zimbabwe hawana noti yao, hawana fedha yao, ni Taifa ambalo limepoteza hata identity. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri, ni muhimu sana mkamshauri Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia suala la Acacia Mining, linaonekana linapongezwa na kila mtu, lakini consequences zake; leo tuna taarifa kwamba Acacia wanakwenda Mahakamani London. Concequences zake Taifa hili litakuja kuingia kwenye gharama kubwa kama lilivyoingia kwenye ile minofu ya samaki na meli kule Dar es Salaam. Kwa hiyo, ni muhimu tukajenga mahusiano. Siasa na biashara ni vitu vinavyofanana. Mwanasiasa imara, mwanasiasa makini ni mwanasiasa atakayejua maana ya uchumi. Hawa wananchi wanaoshangilia leo, baada ya miezi miwili, mitatu watakosa chakula; wakishakosa chakula itakuwa rahisi kuingia barabarani kuliko wangeingia barabarani kudai mikutano ya hadhara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunashangaa mnafanya nini? Leo uchumi umeyumba. Ukienda hapo Kenya, tumemwona Uhuru Kenyatta amekwenda kwenye mkutano wa G7 Summit. Uhuru anakwenda ku-present paper kuhusu Taifa lake. Leo Peugeot wameweka plant yao kule Kenya, kiwanda cha magari kinakuja Kenya. Unajiuliza, hivi kweli Wizara ya Mambo ya Nje inafanya nini? Ukienda kwenye Ubalozi, Mabalozi wanalia. Kama mishahara yao haifiki kwa wakati, wanawezaje wakafanya hiyo connectivity ya kupata wawekezaji kuja huku? Kitakachoondoa wawekezaji, hata hii bajeti mnayopitisha, mimi mwenyewe ningekuwa ni mwekezaji, nasikia mambo mnayoyafanya kwa hizi multinational companies, ningevuta subira kwanza nione hali inakuwaje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ni shahidi kwamba Wazungu wanapokuja kufanya investments za mabilioni, wanaangalia pia future ya nchi hiyo kisiasa. Leo nchi hii masuala ya kidemokrasia yamepigwa marufuku, leo nchi hii mikutano ya hadhara imepigwa marufuku. Maana yake, kwa investor yeyote ambaye yuko serious anataka kuja kufanya investment ya hela nyingi atasema Taifa lile hawana political stability. Maana yake ni nini? Maana yake hawatakuja…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)