Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nimshukuru Mungu kwa nafasi hii na pia nimpongeze Waziri na timu yake kwa kazi ambayo wameweza kuifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwanza na Mamlaka ya Mapato (TRA), suala la EFD. Niliwahi kuzungumza ndani ya Bunge hili kwamba TRA katika kudhibiti mapato na kuweka uwazi, Serikali ilianzisha EFDs na ESDs, lakini kilichopo ni kwamba tuna matatizo ya kimtandao kwenye hizi mashine, kwa hiyo tunaomba TRA iweze kuangalia. Katika uhasibu tunajua katika kurekebisha mahesabu ya kiuhasibu unatoa credit note au debit note, sasa hizi signatures hazichukui taarifa za marekebisho ya kiuhasibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine lililopo TRA, tunapata malalamiko sana kutoka kwa wafanyabiashara kuhusu wanavyofanya makadirio. Wenyewe wako ofisini lakini na mteja mwenyewe ndio anajikadiria kama anavyotakiwa kufanya, lakini wanakadiriwa kwenye hali ya juu tofauti na uhalisia wa biashara walizonazo. Kwa hiyo, tunaomba TRA waangalie ikiwezekana waangalie na hali halisi ya biashara mtu anayoifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya majukumu ya Wizara hii ni kufuatilia mapato, lakini tunaomba, bajeti ya mwaka jana tumezungumza, kuna ripoti nyingi na Kamati ziliundwa na Bunge hili huko nyuma na maarufu sana ripoti ya Mheshimiwa Chenge, kuna Chenge One na Chenge Two. Sasa hizi mpaka sasa hivi kama Wizara wamefanyia kazi kiasi gani? Tunaomba Wizara zote kwa ujumla ziweze kufanya mawasilisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusuukusanyaji wa
property tax ni majukumu ya TRA, lakini nimeangalia katika website katika ripoti yao makusanyo wameweka mwezi Novemba, 2016 tu, sasa je, mpaka sasa hivi wamekusanya kiasi gani, tutaomba Waziri wakati wa majumuisho utueleze upande aw property tax TRA wameweza kufanikisha kiasi gani kwenye makusanyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ukiangalia kwenye ripoti za TRA kuna maeneo VAT baadhi ya categories sijaona wameripoti makusanyo, je, hatuna makampuni yanayo-fall kwenye hizo categories? Kwa mfano electrical products, alluminium, motor vehicle spares and bicycle, sijaona kwenye VAT on local, hawajaripoti. Kwa hiyo, tutaomba tupate kujua nini wanachotarajia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna uandaaji wa mahesabu, TRA wakija kukagua kuna wakati wanahitaji ushahidi wa risiti, lakini sasa hivi dunia imekuwa inaenda kimtandao zaidi. Kwa mfano, unaweza kulipia umeme, kununua airtime kwa kutumia Tigo Pesa, M Pesa, sasa unavyoandika mahesabu yako unaweka reference ipi ambapo yeye staff wa TRA atakuja aridhike kwamba kweli muamala huu uliufanya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutaomba Waziri haya malipo ya sasa hivi ya miamala kwenye gharama zetu za uendeshaji atueleze Serikali wataridhika kwa maandishi yoyote ambayo mtu atasema alilipa kwa Tigo Pesa, M Pesa, Halopesa au Airtel Money au kwa njia nyingine za kibenki kwa njia ya simu, kwa hiyo tutaomba utueleze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mafao, watumishi wa Posta walipandishiwa mafao toka shilingi 50,000 mpaka 100,000 Julai, mwaka 2015 lakini kuna baadhi mpaka sasa hawajaanza kulipwa. Waziri, tutaomba majibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la PPRA, tuna Sheria ya Manunuzi ya mwaka 2011, kuna kipengele cha 77(4) mambo ya liquidated damage na ukienda kwenye regulation ya mwaka 2013 naomba PPRA watupe mwongozo mzuri, wanavyoandaa zile Standard Tender Documents kwenye general conditions zinatofautiana kabisa juu ya liquidated damage na sheria mama pamoja na kanuni. Kwa hiyo, tutaomba Mheshimiwa Waziri tutahitaji majibu kwa nini zinatofautiana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nachangia bajeti ya Wizara ya Kilimo, nilizungumzia kuhusu Benki ya Maendeleo ya Kilimo, Serikali mpaka sasa haijaongeza mtaji, Mheshimiwa Waziri tutaomba utuambie ni lini Serikali itaongeza mtaji kulingana na maazimio ambayo yamekuwa yakizungumzwa huko nyuma. Pia hii Benki ya Maendeleo ya Kilimo ndiyo ambayo itasaidia mtaji kwa wakulima na tunajua asilimia 67 ya wananchi wanajishughulisha na kilimo, sasa malengo ya hii Benki ya Maendeleo ya Kilimo ni yapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa na juhudi miaka yote, tulikuwa na CRDB, haikufanya vizuri matokeo yake imekuwa benki ya kibiashara. Huko nyuma baada ya uhuru tulikuwa na Agricultural Credit Agency iliweza kutoa matrekta. Sasa leo hii benki hii ya kwetu na niliangalia kwenye website yao kwamba wanapata fedha kutoka African Development Bank, je, wamekwishapata hizo fedha? Kwa mfano, Jimboni kwangu nina wakulima wa tumbaku, wanatarajia wakope fedha kwa ajili ya shughuli zao katika riba ambayo itakuwa ni ndogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie pia kuhusu Tanzania Investment Bank, hii inamilikiwa na Serikali, ni kweli kuna benki kama NMB Serikali ina asilimia 31 ya hisa lakini je, taasisi nyingine za Serikali zinashawishiwa vipi kwenda kufungua akaunti huku TIB ili waongeze mzunguko wa fedha na ndiyo benki ambayo inasaidia hata mashirika yetu. Kwa mfano TRL wamekopeshwa fedha na TIB wameweza kuinua operations zao. Kwa hiyo, ni jinsi gani sasa pia taasisi nyingine za Serikali ziweke fedha zao TIB na pia na yenyewe iweze kukua kama ambavyo tunasisitiza upande wa NMB.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba Waziri pia atakapokuja, katika kitabu chake amezungumzia kuhusu mitaji inayozidi, nafikiri hizi ni taasisi mbalimbali za Serikali ambazo sasa hivi zinapeleka fedha zake BOT baada ya kuondoa zile gharama sasa ni mitaji inayozidi. Mpaka Machi, wameweza kupeleka ziada shilingi bilioni 182 ambayo ni sawa na asilimia 24.1 lakini malengo ikiwa ni shilingi bilioni 756, tuna upungufu wa shilingi bilioni 574.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Serikali ni kwamba hii mitaji inayozidi tumezungumza humu tunaomba tulenge kwenye maji. Tuweke kwenye upande wa maji ili Wizara ya Maji na Umwagiliaji ipate vyanzo vingine vya fedha yenye uhakika kwenye hii mitaji inayozidi, iende kwenye maji ambacho ndicho kigezo kikubwa ambacho wananchi wetu wanataka kukiona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijikite kwenye madeni ya huduma mbalimbali pamoja na watumishi. Kumekuwa na malalamiko sana, wafanyabiasara wengi wanadai Wizara zetu miaka mitano, miaka minne, mpaka sasa hawajalipwa. Sasa Serikali kulipa haya madeni ya ndani tutaomba Waziri utuambie una mkakati gani juu ya kulipa madeni ya ndani? Kuna watu wamefanyakazi walikopa, wamekuwa-charged riba, kuna wengine wamepeleka mpaka kwenye Mahakama ya Kibiashara, Serikali ina-charge interest, sasa hizi gharama za Serikali kuendelea kuchajiwa riba kwenye haya madeni, Serikali ina mpango gani wa kulipa haya madeni ya ndani ili na mzunguko wa fedha katika nchi yetu uweze kuendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkaguzi wa Mahesabu ya Serikali (CAG). CAG amefanya kazi nzuri sana na ameweza kutoa ripoti mbalimbali na vitabu tumeviona. Mimi tu nitoe ushauri kwa upande wa Ofisi wa CAG, kuna baadhi ya watendaji katika auditing yao nimewahi kuwauliza, nilikuwa kwenye Kamati ya LAAC, wakati wa audit tunajua audit is all about analytical review, kuna baadhi ya watendaji hawafanya analytical review na ndiyo audit inapo-base hapo. Unaweza kulinganisha, ukilinganisha tu mahesabu ya miaka miwili/mitatu na maongezeko, pale unaweza kujua kwamba hapa kuna upungufu kiasi gani au udhaifu kiasi gani, kwa hiyo niombe Ofisi ya CAG hili waweze kuliangalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwa upande wa Ofisi ya CAG teknolojia ya sasa hivi ime-advance, kampuni nyingi za auditing kama KPMG, PWC, Deloitte & Touche na wengine, wameweza ku-advance kwenye technology wana-audit, wanasambaza mafaili, sasa na hii Ofisi yetu ya NAO na yenyewe huku Serikali itoe fedha ya kutosha na kwa wakati ili wapate training na kuwekeza kwenye technology. Kwa hiyo, uwezeshaji upande wa Ofisi ya CAG uendelee kuwezeshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mafunzo pia kwa wakaguzi wetu, kwa mfano upande wa Halmashauri wanakagua miradi ya maendeleo, wanajua kusoma vizuri BOQ (Bill of Quantities), wanajua kulinganisha? Kuna mahali unakuta kuna variation unakuta Ofisi ya CAG know how inakuwa haipo, tunaomba waweze kupata mafunzo kwenye hayo maeneo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, today I am too very faster. Jambo lingine naomba nirudi upande wa TRA, huko nyuma mtu alikuwa akisimamisha biashara anaambiwa andika barua, lakini sasa hivi wanasema sheria ilikuwa haisemi vile, lakini ndani ya Taasisi hiyo ya TRA wanakwambia unatakiwa ulete nil return, halafu mtu anaku-penalize karibu shilingi milioni 15, shilingi milioni 20 na mtu hakufanyabiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunaomba huku TRA kama mtu hakufanya biashara na mlimbwambia aandike barua, leo hii mnamwambia alitakiwa alete nil return, how come ofisi hiyo inatoa maelekezo mawili? Basi hawa watu wasamehewe, kama Waziri kwa mamlaka yako tutaomba utoe maagizo watu ambao hawakufanya biashara na leo hii wanakuwa assessed kodi pamoja na interest na ma- penalty waweze kusamehewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja. Ahsante sana.