Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE: SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii adhimu kwangu ya kuchangia bajeti hii ya Ofisi ya Makamu wa Rais na nitaomba tuchangie na sisi wengine tutachangia kitaalam zaidi kuliko kisiasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashukuru sana wananchi wa Jimbo langu la Uzini, walioniwezesha leo hii kuweko hapa ili kutoa mchango wangu huu katika Ofisi ya Makamu wa Rais na hasa kwenye upande wa Mazingira. Hali ya Tanzania ni tete, bado hakujawa na mikakati ya utekelezaji wa Sera na miongozo mbalimbali, kwa ajili ya kuhami mazingira yaliyopo. Nchi hii miaka 20 na miaka 10 iliyopita sivyo ilivyo leo, kila siku zikienda nchi inakwenda na maji na kama hakutakuwa na uthubutu wa udhibiti wa mazingira tuliyonayo baada ya miaka 10 hapa tutakuwa hatuna tofauti na wale wenzetu wa Ethiopia na nchi nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala zima la uharibifu wa mazingira lakini vilevile na kuondoka kwa uoto wa asili kwa maeneo mbalimbali tuliyonayo katika nchi yetu, miaka 20 iliyopita katika mabonde ya Usangu, ukija mpaka Mlimba na Iringa, yalikuwa ni mabonde ambayo yanaitwa ni mabonde chepe, leo hii maeneo yale yameharibika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hali ni mbaya zaidi katika Kanda ya Ziwa, hali ya hewa imebadilika, joto limepanda, miti hamna, hali imekuwa ni ngumu zaidi. Ushauri wangu kwa Wizara hii ni kwamba kuwepo na mkakati maalum wa kurudisha uoto wa asili na hasa kwa maeneo yale ya Kanda ya Ziwa na Mikoa ya Kati hapa. Nakuomba Waziri na Waziri Mkuu, uwepo mkakati wa kupanda miti, kwa Watanzania wote, angalau miti minne kwa kila Mtanzania kwa kila mwaka. Mkakati huu ukiwekwa sahihi, tutaweza kuwa na uhakika wa kurudisha hali ya mazingira tuliyonayo. Pia kuweko na aina maalum ya miti ambayo inaweza kuongeza kiwango kikubwa cha uzalishaji wa carbon katika maeneo yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeelezwa katika taarifa iliyoletwa hapa na Waziri kwamba uharibifu uliopo uko wa asilimia mbili, latest information na hasa ile taarifa iliyotoka Durban iko zaidi ya hapo. Kila siku tunapokwenda Ozone Layer inazidi kumomonyoka na ndiyo maana joto linapanda na linashuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka mitano iliyokwisha Dodoma kipindi hiki tulikuwa na baridi leo hii tuna joto na hatuna uhakika kwamba itafika mwezi wa saba baridi itarudi kama vile ilivyokuwa, nchi inakwenda na maji!
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati huu nataka kuunganisha na ule Mfuko aliousema Waziri wa Mazingira, ule ndiyo ukombozi wa nchi hii. Mheshimiwa Waziri nikushauri kitu kimoja, tuanzishe kwa maksudi Mfuko huu na upitie kwenye simu zetu. Kila Mtanzania mwenye simu angalau achangie nusu shilingi katika Mfuko wa Mazingira. Kwa kila sh. 1,000 itaweza kutusaidia utekelezaji wa mbinu mbalimbali za kuweza kuokoa maeneo yale ambayo yameathirika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri mwingine ni kwamba, Mheshimiwa Waziri nakuomba sana urudi kwenye mkakati ule uliotengenezwa na NEAP ambao ulikuwa chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais. Ule Mpango Mkakati na action plan ya NEAP itaweza kututoa kuhakikisha kwamba tunakuwa na mfumo mzuri wa ufugaji, mfumo mzuri wa kilimo, mfumo mzuri wa viwanda na mfumo mzuri wa kuhakikisha kwamba, kila idara inaweza kushiriki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mazingira, Wizara zote ni wadau, suala la mazingira ni mtambuka, hivyo kila Wizara inastahili kuweka fungu maalum kuchangia katika Mfuko wa Mazingira. Wizara ya Madini maeneo mengi yanayochimbwa mashimo ya madini hakuna mpango mkakati wa kuyarudisha kama yalivyokuwa, basi isiwe kurudisha lakini kuweza kuyafanya yale maeneo kutumika kwa shughuli nyingine. Mfumo wa Kilimo tunaolima unasababisha ardhi iondoke rutuba, uoto wa asili unapotea na hali ya hewa inazidi kuwa disturbed, uzalishaji kila siku unaendelea kuwa chini. Hofu yangu kama hakutakuwa na nia thabiti ya kudhibiti mazingira haya, Tanzania itafika mahali itaomba chakula. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile katika kuangalia suala zima la uharibifu wa mazingira katika bahari, Tanzania imezungukwa upande mmoja na bahari, lakini kule Zanzibar tumezungukwa na bahari kila pembe. Bado sijaona udhibiti au mkakati maalum wa kuvinusuru visiwa vile na kuinusuru hii nchi upande wa bahari na hali ya mmomonyoko unaokwenda siku hadi siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa zilizopo za utafiti, kila mwaka bahari inasogeza nusu mita mpaka mita moja juu ya ardhi, kwa hiyo eneo tulilonalo linazidi kupungua, ukiangalia miaka 20 ijayo maeneo mengi ambayo sasa hivi yanakaliwa na watu yatakuwa yamehamwa na maji yatakuwa yamechukua nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taasisi zetu za NEMC na zile zinazofanya impact assessment za kutoa vibali vya ujenzi wa mahoteli na vitu mbalimbali katika maeneo yetu ya bahari, zimekuwa nazo zinatumika kuchangia uharibifu wa mazingira badala ya kunusuru. Nitoe mfano mmoja, tumekuwa na kawaida mahoteli mengi ya Waitaliano yanajengwa…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.