Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuchangia hoja hii ya bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema kwa kutufikisha hadi leo tukiwa katika hali ya uzima na usalama.
Pia napenda sana kuwashukuru wanawake wa Chama cha Mapinduzi wa Mkoa wa Kusini Pemba kwa kunichagua kwa kura za kishindo na kuniwezesha kuwa Mbunge wao, nawaahidi sitowaangusha kama kawaida yangu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nianze kwa kuipinga ripoti ama hotuba ya Kambi ya Upinzani, ambayo ameisoma Mheshimiwa Ally Saleh, kusema kwamba Zanzibar uchaguzi ulikuwa mbaya, wananyanyaswa, ushindi hawakupata CCM, wao ndiyo waliopata ushindi, wamenyang‟anywa ushindi, mimi niwaulize ushindi huo waliupata wapi? Kupata ushindi siyo bure, kupata ushindi ni kazi, kwa hiyo, naomba tu tustahimiliane. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napenda kwenda moja kwa moja katika bajeti. Kwanza napenda kuipongeza Wizara hii na Mawaziri wetu wa Wizara hii Mheshimiwa January Makamba na Mheshimiwa Mpina, Mwenyekiti wangu wa Wilaya, alikuwa Mwenyekiti wa Vijana wa Wilaya, nilipokuwa Naibu Katibu Mkuu wa Vijana. Nawapongeza sana kwa kazi kubwa mnayoifanya kwa ushirikiano mzuri, nawatakia kila lenye kheri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda sana kuupongeza uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2015, kwa ushindi wa kishindo ambao tumepata Chama cha Mapinduzi, tukawa tunaongoza Serikali ya Chama cha Mapinduzi inayoongozwa na Dkt. Pombe Magufuli. Uchaguzi wetu Mkuu ambao ulifanyika kwa kule Pemba CUF walipata huo ushindi, lakini nashangaa wanasema nini na wao wamo humu ndani? Mnasema hamuukubali Uchaguzi Mkuu mbona ninyi mmo humu ndani hamtoki, au mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu? Kwa sababu kama hamuutambui uchaguzi ule, mngetoka mkaenda majumbani mwenu, mmo humu, mnachukua posho, mnafanya kila kitu hapa, lakini hamuukubali uchaguzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Mama Samia Suluhu Hassan, wanawake tunaweza. Mama huyu ni fighter, anafanya kazi usiku na mchana katika Serikali hii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tunakupongeza Mama Samia. Pia napenda kumpongeza Waziri wetu Mkuu Majaliwa mtu wa watu, mtu wa vitendo, jembe hongereni sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda sana kuupongeza uchaguzi wa marudio wa Zanzibar, Uchaguzi ambao umekuwa wa demokrasia, uchaguzi ambao Vyama vya Upinzani ambavyo vimeshiriki uchaguzi huu wa marudio, wa tarehe 20/3/2016, Chama cha ADC, chama cha TADEA, Chama cha Wakulima, vilishiriki uchaguzi huu wa marudio, CUF wao na chama cha CHADEMA wakapingana na uchaguzi huu wa marudio na lazima waukatae Uchaguzi huu, kwa sababu uchaguzi wa Oktoba, 2015 waliiba kura.
MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa wamezoea bobo hawa, bobo kama hulijui nitakwambia. Napenda kuupongeza uchaguzi huu wa marudio chini ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar iliyoongozwa na Mheshimiwa Jecha.
MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Jecha hongera popote ulipo, kwa kusimamia Uchaguzi wa Zanzibar kwa amani na utulivu na usalama. Jecha hoyee!
MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, uchaguzi huu uliompatia ushindi Mheshimiwa Rais wetu Mtukufu, Ali Mohamed Shein, Rais jasiri, Rais mstahimilivu na kama Rais siyo mstahimilivu basi angekwishakufa kwa hawa Wapinzani, lakini Mheshimiwa Dkt. Shein ni Rais jasiri, ameiweka Zanzibar katika amani na utulivu. Vile vile tunavishukuru Vyombo vya Usalama wa Taifa, vyombo vya Muungano.
MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Ally Saleh kaa kitako nikueleze, ninyi mlipokuwa mnasema nilinyamaza, sasa na mimi nasema ni bosi wenu wa Chama cha Mapinduzi nasema nataka mnyamaze!
MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilindie muda wangu tafadhali, nina mambo mengi ya kusema hapa leo. Pia nampongeza Balozi wetu Seif Idd, ni Kiongozi bora.
MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Ninyi hamumtaki kwa sababu anawatia adabu, Muungano wa Zanzibar na Tanganyika, Oyee!!!!
MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashukuru Mwenyezi Mungu kutujalia Muungano huu, ulioasisiwa na Hayati Abeid Amani Karume na Hayati Julius Kambarage Nyerere, Mwenyezi Mungu awalaze mahali pema Viongozi wetu shupavu.
MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, Muungano una maendeleo mengi sana, Wazanzibari tuko kila pembe ya Mikoa ya Bara, tunafanya biashara, tumeoana, tunashirikiana.
MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.