Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa niipongeze Wizara ya Fedha kwa hotuba yao nzuri iliyojaa matumaini makubwa. Naomba niishauri Serikali katika suala zima la road license, ni ukweli usiopingika kwamba Serikali inatakiwa ikusanye mapato ya kutosha ili nchi iweze kujiendesha yenyewe, lakini mimi kama Mbunge nimegundua tunakosa mapato mengi kwa kulipia kila gari, ikizingatia magari mengi yamekufa na mengine yamekatwa skrepa, Serikali inayavizia iyaone barabara ili yakamatwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa ukusanyaji huu tutakuwa tunapoteza mapato mengi sana. Niishauri Serikali iongeze hata shilingi tano kwenye kila lita ya mafuta, ukipigia hesabu ya kila gari kwa mwaka itakuwa imelipia fedha nyingi sana, itakuwa mara kumi ya ukusanyaji huu unaotumika sasa, kwa kufanya hivyo Serikali itagundua ilikuwa inapoteza fedha nyingi sana kwa mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali yangu kuhusiana na TRA. Kila TRA hasa za Wilaya zipandishwe hizi ziwe zinatoa huduma zote mfano TIN namba road licence.

leseni za udereva, motor vehicle na kadhalika. Serikali ikifanya hivi itaongeza mapato mara dufu kuliko ilivyokuwa sasa ukizingatia wananchi walio wengi wanaishi vijijini, anaona ngumu kwenda kukata leseni mkoani hivyo yupo tayari aendeshe chombo cha moto kwa kujificha ili mradi asitumie gharama kwenda kutafuta vitu hivyo. Kwa hiyo, Serikali imekosa mapato kwa kutopeleka huduma karibu na wahitaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuhusu wafanyabiashara. Mfanyabiashara anakadiriwa mapato wakati hata hajafungua biashara. Niishauri Serikali ishawishi watu wafungue biashara kisha baada ya mwaka ndipo anafanyiwe makadirio kama sheria inavyosema. Sasa hivi TRA na wafanyabiashara ni kama maadui wakati Maafisa hawa wanatakiwa wawape elimu wafanyabiashara ili Serikali iweze kupata mapato au kukusanya mapato mengi zaidi kuliko ilivyokuwa sasa Maafisa wa TRA wanawatisha mno wafanyabiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mashine za EFD, mashine hizi hazitumiki kama ipasavyo hasa katika Halmashauri zetu, kuna wizi mkubwa sana unafanyika katika Halmashauri baadhi kwani watendaji wengi wa Halmashauri wanatoa maelekezo kwa maafisa wanaokusanya ushuru kuwa kuna sehemu za kutumia risiti za EFD na sehemu nyingine wanatumia manual, hii inasababisha upotevu wa makusanyo na kuitia Serikali hasara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu katika Halmashauri nyingi hapa nchini hasa zile zinazotiliwa mashaka zifanyiwe ukaguzi wa mara kwa mara (special auditing), mfano Halmashauri yangu Lushoto inakusanya mapato mengi lakini mwisho wa siku unaambiwa mapato yameshuka. Mimi kama Mbunge napata mashaka sana na kama mnavyojua Halmashauri ya Lushoto ina wakulima na wafanyabiashara wengi, haingii akilini ukiambiwa kwa mwaka Halmashauri imekusanya asilimia 38 tu wakati huo unaona kuna vitu vya hovyo vinafanyika bila kufuata taratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Halmashauri ya Lushoto ikafanyiwe special auditing, mimi kama Mbunge nimeliona hilo.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mjaalie afya njema na umzidishie umri ili aendelee kuwatumikia Watanzania hasa wanyonge wa nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.