Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Othman Omar Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Gando

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. OTHMAN OMAR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nachukua fursa hii kuipongeza hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani kwa ushauri ilioutoa juu ya kuishauri Serikali katika suala zima la kuleta maendeleo ya uchumi ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia kero za taasisi tatu ambazo binafsi napenda nipate ufafanuzi wa Waziri mwenye dhamana. Mapato yatokanayo na AICC. Katika kikao cha 10 cha Mkutano wa Sita cha tarehe 10 Februari, 2017, Waziri wa Fedha nilimnukuu wakati akijibu swali la pili la nyongeza lililoulizwa na Mheshimiwa Ali Saleh kutokana na swali la msingi Na. 110 ambalo lilihusu ruzuku ya Zanzibar kutokana na Shirika la AICC. Mheshimiwa Waziri wa Fedha alijibu kama ifuatavyo nanukuu:

“AICC haijawahi kupata gawio kwamba Joint Finance Commission na Ofisi ya Msajili wa Hazina wameunda kikosi kazi ili kusaidia kituo kupata faida na kuleta gawio Serikalini kuanzia mwaka ujao wa fedha”.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa hii ya Waziri wa Fedha inakinzana na taarifa za shirika la AICC, taarifa ya Waziri wa Mambo ya Nje na zile za Msajili ya Hazina. Taarifa ya AICC inaeleza kwamba shirika linajiendesha kwa faida na ufanisi mkubwa na kwamba halitegemei ruzuku ya Serikali na linachangia kwenye Mfuko wa Serikali. Naomba ufafanuzi wa kina kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha kuhusu mchango wa mapato ya AICC Serikalini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), TRA inaleta usumbufu kwa Wazanzibari, unapoingiza bidhaa kwenye ardhi ya Tanzania Bara kutoka Zanzibar ushuru wake unalingana na bidhaa zinazotoka nchi nyingine. Ushuru wa bidhaa unaodaiwa na TRA na ZRB kwa mfanyabiashara wa Zanzibar inamfanya mtafuta riziki huyu kutoa ushuru mara mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi ni baadhi ya kero ambazo zinawakandamiza Wazanzibari na zinazowarudisha nyuma kiuchumi. Naomba ufafanuzi wa Waziri wa Fedha kuhusiana na TRA kwa wananchi wa Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Benki ya TADB tayari imeshatoa elimu ya matumizi ya benki hii na tayari imetoa mikopo na kupokea maombi ya mikopo kwa wananchi wa Tanzania Bara. Jambo la kusikitisha, Benki hii licha ya kuwa haijafanya mambo hayo Tanzania Visiwani hata kujulikana na wananchi wa Zanzibar hawaijui.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamwomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha apeleke huduma ya TADB Zanzibar kama huduma hii inavyotolewa kwa upande wa Tanzania Bara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.