Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, kaka yangu Mheshimiwa Philip Mpango kwa kazi nzuri na nampa pole kwa changamoto kubwa za kuendesha uchumi wa wananchi. Pia napenda kumpongeza Naibu Waziri, Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji. Napenda kuwapongeza watendaji wote chini ya Katibu Mkuu, Ndugu James Dotto pamoja na Manaibu wake. Jimbo la Nyasa tunawashukuru sana kwa support mnayotupa, tunasema ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina jambo dogo kuhusu kufungwa kwa Benki ya Mbinga, napenda kujifunza tatizo ni nini? Benki ile ilikuwa inasaidia sana wakulima wadogo wadogo hasa katika mikopo. Najua kulingana na hali halisi huenda running costs zilikuwa kubwa au uendeshaji usio na tija (ubadhirifu) sasa sijui ni nini kilichotokea. Kwa kuwa wananchi wameulizia sana, naomba kupata majibu na hasa juu ya hisa zao. Nawaombeni na naamini jitihada zenu zitaendelea kuzaa matunda.