Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kwanza kabisa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya na baraka zake kwetu. Naomba nichukue fursa hii kumpongeza Waziri, Naibu Waziri pamoja na Katibu Mkuu akiongoza timu yake ya wataalam kwa kazi kubwa na nzuri wanayofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ndiyo Wizara mama ambapo Wizara zote zingine zinategemea ufanisi wa Wizara hii. Naamini Wizara ya Fedha inaweza kufanya vizuri zaidi ili matumaini ya Watanzania yaweze kutimia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nishauri Waziri wa Fedha alete mabadiliko ya sheria Bungeni kumrudishia uwezo wa kutoa msamaha wa kodi katika miradi mbalimbali na pia katika misaada tunayoweza kupata kama Serikali, taasisi zinazotoa huduma na Halmashauri zetu. Naamini tulikosea kufuta uwezo wa Waziri wa Fedha kutoa msamaha wa kodi. Kelele nyingi za wawakilishi na pia taasisi zetu kupunguza masuala ya kodi siyo katika hii miradi na misaada midogo, walikuwa wanalenga misamaha mikubwa kama ya kwenye migodi, utafutaji wa madini (research) na uchimbaji wa madini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii imekuwa kero tukipata misaada kutoka kwa wafadhili ambao hawako tayari kutoa au kulipia kodi, mfano magari ya wagonjwa, miradi ya maji, madaraja, ujenzi wa hospitali na vituo vya afya, huduma za elimu na zingine. Muhimu ni kuweka wazi misamaha hiyo na tulio wengi tusiadhibiwe kwa ajili ya wachache waliofanya vibaya kwa kutumia vibaya mfumo wa msamaha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nishauri Wizara iongeze wataalam zaidi katika Idara ya Mipango. Idara hii ndiyo inayoweza kuleta mafanikio makubwa sababu ya kushauri kwenye sera na pia kuboresha mapato ya Serikali hasa kutanua wigo wa kukusanya kodi (tax base).

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri waajiriwe wataalam hasa kutoka private sector wenye uzoefu ili kuleta mabadiiko ya fikra (mind set change) ndani ya Wizara. Jukumu la Wizara ni kusimamia kukusanya mapato yote ya kikodi na yasiyo ya kikodi pia matumizi ya mapato hayo pamoja na kuweka mipango ya miradi ya maendeleo. Kwa sasa sera yetu imefanya Tanzania iwe moja ya nchi ambapo sekta isiyo rasmi (informal sector) kuendelea kukua kwa kasi na formal sector kuendelea kushuka. Hatukusanyi kodi katika sekta isiyo rasmi na kuumiza sekta rasmi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Wizara iangalie uwezekano wa kuleta mabadiliko ya sheria ambayo itaweka muda wa ukomo wa kodi, tozo au ushuru ambayo haijakusanywa kwa muda maalum na siku mkusanyaji akizinduka usingizini anataka alipe kutoka siku sheria ilipotungwa. Sio kila mwananchi anajua sheria, ni wajibu wa Serikali ngazi zote kutafsiri sheria na kutoa elimu kwa wakati. Kwa sasa wananchi wanalalamika sana, pamoja na baadhi za Halmashauri kutoza kodi, tozo za miaka mingi iliyopita, uzembe wa kutokusanya wakati huo siyo wao. Mfano ni Motor Vehicle License, SDL, Withholding Tax na je, hao waliosababisha kutokukusanya wamechukuliwa hatua gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri Wizara iangalie namna ya kuongeza fedha katika taasisi zilizo chini yake kuna TADB na TIB. Pia kupitia Sheria ya Kodi kuleta mabadiliko ya kupunguza kodi mbalimbali ili compliance iwe kubwa na fine na adhabu kwa watakaodanganya iwe kubwa. Wizara iangalie namna ya kuhakikisha mifuko iliyokuwa chini yake kama Mdhibiti wa Mahesabu ya Serikali na Mkaguzi Mkuu (CAG), Mahakama na Bunge zifanyiwe utafiti zaidi ili kazi zao kama mihimili tofauti na huru zifanikiwe. Pia Msajili wa Hazina, Kitengo cha Utafiti na Uendelezaji (R&D) kiboreshwe ili taasisi zote chini yake ziweze kuleta faida na kuchangia katika uchumi wa Taifa letu.