Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante. Mbunge wa Msalala amenifurahisha anasema nchi inaibiwa kwa hiyo kama nchi inaibiwa, basi lazima tuzuie isiibiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naunga mkono hoja hii na nimpongeze Waziri Dkt. Mpango na Naibu wake hongera sana wanafanya kazi kubwa. Pia niwapongeze wataalam kwenye Wizara yake, Gavana wa Central Bank Profesa Ndulu wanafanya kazi nzuri hasa katika mazingira haya mapya ambayo muda wote tumekuwa tukiibiwa na watu wengi wamekuwa hawalipi kodi. Dkt. Mpango wako vizuri hongera, wachape kazi, changamoto ni nyingi lakini huo ndiyo mwendo. Mzee Mwinyi Rais wa Awamu ya Pili alisema kwamba “kila zama zina kitabu chake” sasa zama hizi ni mpya lazima tucheze ngoma kadri inavyopigwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo mawili tu ya haraka haraka, kwanza; Mheshimiwa Waziri namkumbusha ujenzi wa Ofisi za TRA – Kasulu, kwa maana kwamba huduma za TRA pale Kasulu ili mtu akafanye registration ya gari akitoka Kakonko, Kibondo, Buhigwe na Kasulu anasafiri kwenda Kigoma. Bosi wa TRA pale anasema shida yao ni mashine kwamba kuna mkubwa mmoja alikuwa haja-release mashine zile kwenda pale Kasulu ili wawe wanafanya registration ya magari. Nimepata taarifa sasa hivi kwamba registration ya TIN-number wameanza last week, hilo ni jambo jema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Waziri nimkumbushe kwamba Halmashauri ya Mji wa Kasulu tumeshawapa kiwanja TRA, tunaomba wajenge Ofisi sasa. Wanapanga kwenye vijumba vya hovyo hovyo pale, wakati nina uhakika TRA wana uwezo wa kujenga Ofisi pale. Tunataka Ofisi ya TRA tumewapa kiwanja, tunaomba wajenge Kasulu kwa Wilaya zote nne ambazo zinazunguka eneo lile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hilo, niseme lingine dogo, Waziri naomba alisikie hili, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Kilimo tulikuwa na semina na watu wa SADC na watu wa IFAD na wafadhili wengine, wamelalamika sana wanasema Serikali, Wizara ya Mheshimiwa Waziri, Hazina hawataki kupokea fedha za msaada wa kilimo. Wote tukatazamana tuliokuwepo pale. Wamelaumu kitu kinaitwa Kamati inayopitia madeni sijui kwamba imejaa urasimu, siyo rafiki, sasa tukajiuliza wote, Mwenyekiti wangu ataniunga mkono yule pale ni kitu gani hiki?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu, hebu wakakae na hawa partners wetu, ni kitu gani ambacho kiko Hazina pale mpaka kinasema hawa marafiki zetu wanaotaka kutusaidia kwenye sekta ya kilimo hizo fedha hawazitaki kuzipokea. Actually underline wamesema hawataki kupokea fedha zao na wakaenda mbali zaidi wakasema IFAD wana miradi mitatu, hawataki kupokea fedha zao, World Bank wana miradi mitatu ya kilimo, hawataki kupokea fedha zao, NORAD wana mradi mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliokuwepo pale tukaanza kushangaa pale. Ni kitu gani kinatokea Hazina, fedha za support, zingine ni msaada unakuja, ni kitu gani pale Hazina kinaleta urasimu huo? Tunakwenda mbali zaidi Mheshimiwa Waziri wanalaumu baadhi ya Watendaji wake kwamba wamejaa urasimu na wanatupotezea fedha nyingi katika sekta ya kilimo. Nimelisema hili kwa sababu jana limezungumzwa na wenyewe waliokuwepo pale hebu wawe pro-active basi, fedha zinazokuja wazipokee tuweze kuchapa mwendo kusaidia sekta ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine dogo ni hili, kwenye kitabu ukurasa wa 89 Mheshimiwa Waziri amesema moja ya majukumu kwa mwaka 2017/2018 ya Benki ya Kilimo ni kuwasaidia na kuwawezesha wakulima wadogo. Waziri atakapokuja kuhitimisha atueleze hao wakulima wadogo ni wa wapi watakaowawezesha, watawawezeshaje wakati Benki yenyewe ndiyo hiyo? Wao jana walikuwepo kwenye semina hiyo, walikuwepo watu wa Tanzania Agricultural Bank, nao wanasema wana shida ya fedha. Ningependa hilo nalo Mheshimiwa Waziri aliweke sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja, Waziri chapeni mwendo na wakati ndiyo huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsanteni sana.