Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Riziki Saidi Lulida

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. RIZIKI S. LULIDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru nami kwa kupata nafasi hii. Niungane na Mheshimiwa Ally Saleh kuhusu investment confidence haipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi nilikuwa katika mkutano wa malaria ambao uliandaliwa na USAID na wao wameingia katika uwekezaji katika malaria, ambacho ni kiwanda kimojawapo nataka nikitolee mfano cha A to Z. Kile kiwanda kina wafanyakazi 8,000 kinalipa kodi bilioni 17, kinalipia TANESCO bilioni moja, lakini cha kusikitisha kwa vile hakuna health policy, narudia tena hakuna health policy inayomfanya yule mwekezaji awe na confidence na uwekezaji wake. Kwa mfano, yeye ana kiwanda cha kutengeneza chandarua ambazo zina dawa na zimehakikiwa kimataifa na ndani, lakini leo wanaingiza vyandarua feki kutoka nchi za nje ambazo yule mfanyabiashara analipa kodi, yule anaambiwa kwa vile chandarua tunagawa bure anaingiza bidhaa zile bure. Tunajiuliza, tuko tayari kusimamia viwanda vyetu au bado tunakutana na kipingamizi kikubwa kwa vile hatuna sera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilizungumza hapa kuwa nchi hii bado hatujaingia katika sera ya viwanda na tunakwenda katika viwanda, sera iko wapi? Matokeo yake huyu anaingiza hiki, huyu anaingiza hiki, matokeo yake kiwanda kitakufa, watu 8,000 Watanzania waliopata ajira, zitakuwa zimepotea. Ushuru mkubwa anayepeleka tax ya bilioni 18, huyu anaingiza bidhaa kutoka nje, even price control inakuwa haipo. Tunataka tufanye kazi tukijua tuna idadi ya kiasi gani? Quantity, quality, price na time delivery inatakiwa ijulikane. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama tunakwenda katika uwekezaji wa kiholela bado viwanda vyetu vitakuwa vinasuasua, wanaleta wawekezaji wa nje, ndani watafunga hivi viwanda na tutakuwa hatuna kodi, wala kutakuwa hakuna ajira. Tuwe wa kweli, tusimamie sera, wailete Bungeni
tuifanyie kazi, lakini wakiendelea viwanda, wakati hakuna sera, kutakuwa hakuna biashara wala hakuna maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mdau natoka Lindi, Selous ni mbuga kubwa naizungumzia huu ni zaidi ya mwaka wa kumi, lakini jiulize kama TANAPA, Serengeti ni ndogo inaingiza bilioni 100, Selous hamna kitu ni ubabaishaji, kuna nini hapa? Kwa nini kuna kigugumizi ndani ya Selous? Korido ya Seleous ambayo ina tembo inafanyiwa promotion gani? Hakuna. Wanakwenda kuwakamata akinamama wauza maandazi, wanaouza mitumba mikononi, lakini wanaacha mabilioni ambayo yako katika Selous. Ili nchi hii iendelee tunahitaji uongozi, siasa safi na watu. Sasa kama vitu hivi havisimamiwi kwa pamoja itakuwa hatufanyi kazi ambayo imetuleta hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia tena kuhusu suala la mjusi. Mjusi ukiingia ndani ya exhibition unalipa Euro 24 kwa mtu mzima, kwa watoto wanaingiza kwa Euro 12, lakini kwa mwaka wanaingiza Euro milioni 600. Uki-convert into Tanzanian shillings unapata trilions of trilions. Sisi tunapata nini? Jamani hata tukitaka revenue au kukaa chini tukatengeneza mrabaha, nchi ikajipatia hata angalau bilioni 200 haiwezekani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanafumba macho wanaangalia vitu vidogovidogo pombe, soda, jamani mbona wana mabilioni ya pesa wanayaacha, hawaoni kama wana uchumi mkubwa wanauacha? Wanatuweka Tanzania katika hali ngumu, lakini kumbe hali ya kupata uchumi ipo. Tujiulize, kwani wataalam wanafanya kazi gani? Uchumi huu wanaoukalia wanafanya nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tufike mahali basi tuambiane ukweli kama tumefeli tuseme tumefeli; kama hatujafeli mambo matatu nataka yatekelezwe. Suala la pato la mjusi, suala la Selous na suala la wawekezaji wa ndani kupewa kipaumbele ikiwemo A to Z ya Arusha. Wameweka Mwekezaji, amekuwa frustrated hata kufunga kiwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina mengine nakushukuru sana dakika tano zimenitosha.