Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2017/2018

Hon. Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2017/2018

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa ujasiri aliouonesha kwenye makinikia hayo yaliyoshikwa huko bandarini. Pia nimpongeze kwa ujasiri na kwa bahati mbaya leo Profesa Muhongo hayupo hapa, nilitaka nimkaribishe darasa la saba huwa tunakaa huku ili tuwe tunamfundisha hali halisi ya Watanzania tunayoina kule majimboni, tukaachana na ule u-profesa.

Mheshimiwa Naibu Spika, watu wengi humu wanaopiga kelele wamekaa na wawekezaji na wengine hata dhahabu hawaijui. Wanasema hatujaisoma Sheria ya Madini lakini yeye hajawahi hata kuona madini, anamiliki nyanya, kwa hiyo hivi vitu bora akakaa ili tuzungumze watu tulio na uchungu. Iringa na dhahabu wapi na wapi? Huyu mtu anamiliki nyanya, kuku na mbwa halafu anakuja kuanza kujadili vitu vya msingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimwambie rafiki yangu msomi kabisa tuachane suala la mchanga; anifafanulie na aelewe wizi ambao uko kwenye migodi hii mikubwa. Ukienda kwenye uhalisia kwenye hii migodi ya North Mara ukienda Buzwagi, ukienda Kahama Mining kote kuliko na migodi hii kuna kanembo kadogo kameandikwa ACACIA; na ACACIA ana hisa asilimia 21 kila mgodi na ameziuza kule Uingereza amepata Dola bilioni 275 na Serikali yetu TRA wakaenda kudai kodi, akawaambia mimi sina file kwenu, tumeshinda kesi amekata rufaa. Sasa alichokiuza kule Uingereza ameuza nini? si ameuza North Mara ya Mara, ameuza ACACIA, ameuza Buzwagi ya Kahama, ameuza Kakola? Sasa hawa watu wana kesi nyingi na ndiyo maana Mheshimiwa Rais amesema tuwachunguze. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, halafu kingine, suala hili siyo la Bunge, ni Mbunge gani aliyegundua kama tunaibiwa ule mchanga pale? Ni Mheshimiwa Rais na jitihada zake, acheni akamilishe Tume atuletee humu ndani. Tunaacha kushughulika na mambo ambayo tumelipwa posho kuzunguka kama Kamati tukayaibua sisi wenyewe, mtu kaibua mwenyewe, hajakamilisha uchunguzi wake, ninyi mnaanza kusema anafukuza wawekezaji, anawafukuza wapi? Hii ni mifano tu, hili Bunge siyo lile mlilozoea kwamba mnakaa kule nyie wenye midomo, mnapewa hela kuja kutupigisha makofi, mtazirudisha time hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata wenzangu hawa upinzani wengine humu ndani mnapiga makofi bure wenzenu wamekula hela Morena pale mnataka tuwataje? Acheni watu wafanye uchunguzi tufike mahali Rais atoe mwelekeo. Rais ndiyo ameshika makontena wala hayakushikwa na Tundu Lissu. Nawashangaa Wanasheria mimi siyo Mwanasheria huyu ndiyo Rais. Dira ya Wanasheria wetu inayoongozwa na Rais Tundu Lissu ndiyo hiyo ya kupingana na sisi tunaibiwa? Naomba sana hawa vijana watulie Mheshimiwa Rais afanye kazi, kile ni kichwa acha kishike na mtashikwa na mengine zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kweli huu mchanga wanavyosema wenzetu kwamba ukipelekwa kule Japan wao wanatoa madini ya aina tatu; wanatoa dhahabu, copper na silver. Sasa uchunguzi tu wala hatuhitaji Maprofesa waliohangaika na wanaoendelea kupiga maneno humu ndani, watupeleke kule Japan wakatuoneshe ule mchanga baada ya kutoa yale madini matatu ule mchanga una madini 32 ule unaobaki una nini? Kama una mali tuuze basi kule Japan hata kama wameyafyatua matofali si tutavunja tu hivi, tunapima, tunapata yale madini yetu? Tunapiga hesabu kubwa ambazo hawa hawaelewi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi natokea kwenye hiyo migodi mikubwa, nataka niwaambie ambao hawaijui hata dhahabu. Tunanunua mfuko mmoja wakati hawajaanza kusafirisha na bunduki, vijana walikuwa wanazunguka na wale madereva ukiuziwa kamfuko kamoja karambo ka- Azam kale Sh.800,000 unapata Sh.16,000,000 na tulikuwa tunaiba kweli na watu wamepata hela. Sasa kama hakuna dhahabu kwa nini wanasindikiza na Mapolisi mbele na nyuma na makontena yale yanalindwa hata yakiwa bandarini?

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwaambie Watanzania wajue na kama ingekuwa Mheshimiwa Rais anaweza kupokea ushauri wangu; hawa wanaobwabwaja huku tukawaruhusu wakafanye mikutano kule Kanda ya Ziwa, hamtarudi ninyi, hamjui shida tulizonazo. Tumeibiwa vya kutosha, tumuache Mheshimiwa Rais afanye kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Ole Milya kwa sababu yeye anajua maana ya Tanzanite, anajua tunavyohaingaika, ameunga mkono, achana na hao watu, mtu wa Dar es Salaam na dhahabu wapi na wapi? Mnyika anamiliki mtambo wa kujengea nyumba, hakuna kitu, hawa wanatusumbua watuache, tumemwamini Mheshimiwa Rais afanye kazi

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Muhongo...

KUHUSU UTARATIBU ....

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Waitara asifikiri mimi ni mwoga wa kupokea taarifa, kwa vile umefafanua nilikuwa right tu kuwataja, lakini nitawavumilia. Nimwambie tu kwamba, kwa vile yeye ameona nimesema uongo, anaweza akasimama yeye akatuambia kule African dream aliyelipa posho ni nani kwenye kile kikao kilichofanyika? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunaotoka kwenye machimbo tunaiomba Wizara ya Nishati na Madini, maeneo mengi yamemilikiwa na watu wanakaa Dar es Salaam wala hawayachimbi. Sisi tunapata shida kila mwaka kuomba Wabunge wa Geita na Mungu katupa neema hii. Mheshimiwa Waziri alikuja akatuambia mwezi wa Saba na wa Tisa kuna maeneo yanarudishwa kwa wananchi tunayasubiria.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo nataka niwaambie wako wawekezaji wazawa wadogo tu wamewekeza zaidi ya bilioni 30 migodi kama ya GGM kwa nini Serikali na Wizara yake isiwakuze watu kama hawa? Uko mgodi wa Busolwa Mining, uko mgodi huko Bunda, kwa nini tusijaribu kuwakuza hawa tukaachana na hawa Wazungu wababaishaji? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Geita siku moja ilikuja ile helicoptor kuchukua dhahabu. Ilipofika pale wakazidishia tofauti na mkataba ulivyo, akakataa kurusha helicoptor, lakini TMAA hawa walikuwa wamegonga dhahabu iende kwa kiwango kile kile. Kwa hiyo, hawa wanaopiga kelele hawaelewi jamani nchi inaibiwa wajaribu kuja kututembelea wenzenu tunaachiwa mahandaki. Naliomba Bunge tumuachie Rais kazi hii aimalize, potelea mbali hata kama tunashtakiwa kwani Sheria ni ruler au ni glass kwamba ikidondoka itavunjika? Tukishtakiwa kwani Tundu Lissu asiposhtakiwa ana kazi gani? Wanasheria wetu watafanya kazi tuiachie Serikali na tumuachie Rais, sisi kama Bunge tumuunge mkono na mimi binafsi sijawahi kuona Rais wa ajabu kama Tundu Lissu, huyu ndiyo wa kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.