Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2017/2018

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2017/2018

MHE. COSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba kuanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa ujasiri mkubwa na hasa kwa sababu mimi na Mheshimiwa Rais mwenyewe tunatoka kwenye mkoa ambao hawa wachimbaji wa dhahabu kwa kweli wanatuachia mashimo matupu na watu wanaendelea kuwa maskini. Kwa hiyo, hizi jitihada za Mheshimiwa Rais tunaziunga mkono, tunampongeza sana na wananchi wa Mkoa wa Geita kimsingi ambao wameshuhudia miaka 19 dhahabu inachimbwa lakini Makao Makuu ya Mji wa Geita hakuna barabara, Makao Makuu ya Mji wa Geita hakuna maji, hospitalini hakuna wodi, shule watoto wanakaa chini kilometa moja kutoka kwenye mgodi pale watu ni maskini sana; wanaona juhudi hizi za Mheshimiwa Rais zinatakiwa kuungwa mkono.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nawashangaa sana wenzangu hawa ambao wanapinga kwa sababu kama walivyosema wenzangu huko nyuma, walikuwa kila siku wanalalamika wanasema kwamba nchi hii inaibiwa lakini nataka kusema kwamba Mheshimiwa Rais aendelee na ikiwezekana na aangalie pia katika maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwanza nataka nimkumbushe Mheshimiwa Mnyika katika ukurasa wake wa saba amezungumzia kwamba Serikali iliingia mkataba wa loyalty wa four percent. Hii ni four percent siyo ya force declaration. Unapofanya force declaration, four percent yeyote haina maana yoyote ile kwa sababu unazungumzia four percent ya value gani? Hawa watu wanafanya four percent ya uongo halafu wanakuja kuwatetea hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine la pili; nilikuwa namshangaa sana Mheshimiwa Mnyika kwenye ukurasa wake wa tisa anasema kwamba taswira ya Tanzania kwenye jarida moja huko la Mining journal inasema trouble in Tanzania kwa sababu Rais ameanza kufuatilia wizi, so what? Trouble, yes kuna wizi unagundulika, unataka Rais asigundue wizi? Lazima Mheshimiwa Rais afuatilie kwa sababu unaposema trouble in Tanzania, kama kuna wizi umegundulika lazima Rais afuatilie sasa mimi nakushangaa unapo…

KUHUSU UTARATIBU .....

MHE. COSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, ulichosema ni sahihi na namshangaa sana ndugu yangu hapa mimi nazungumzia issue katika general yake yeye anajaribu kwenda katika eneo dogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa sababu ya muda, kuna mzungumzaji pia mmoja amezungumzia kwamba uzalishaji wa umeme umepungua, nilitaka aende kwenye ukurasa wa 21 ataona mahitaji ya umeme ndiyo yaliyoongezeka kutoka megawats 1,026 kwenda megawats 1,051, lakini uzalishaji wetu ni megawats 1,450.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie nafasi hii kuishukuru sana Wizara hii. Geita tulikuwa tuna matatizo makubwa sana ya umeme, unakatika kila siku; hivi ninavyozungumza sasa hivi umeme wa Geita haukatiki, umeme wa Geita uko imara na ninachowaomba tu sasa hivi ni kuhakikisha sasa umeme huu kama ahadi ambavyo ilikuwa kwamba vijiji ambavyo vilikuwa havijapata umeme wa REA vinapata. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo nataka kusema hapa ni kwamba pamoja na umeme wa Geita kutokatika, lipo tatizo ambalo nilimwambia Mheshmiwa Naibu Waziri kwamba TANESCO hawana vifaa. Kwa hiyo watu wanapoomba umeme wanachukua muda mrefu sana kupata connection ya umeme; hivyo nadhani pamoja na juhudi za REA TANESCO wakae upya wafikirie namna ambavyo wanaweza kuongeza mtaji. Kama TANESCO wameshindwa kuwa na vifaa vya kutosha kwenye store, ni vizuri wakaruhusu vendors wengine wakawa na vitu hivi kwenye maduka na wao wa-control quality kuliko ilivyo sasa, mteja ameomba umeme leo anafungiwa mwezi wa 10 kwa sababu wewe huna meter, kwa sababu wewe huna waya wakati soko hili ni soko huria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huo ndiyo ushauri wangu. Nakushukuru sana kunipa nafasi.